Taarifa zilizotufikia zimeeleza kuwa, msanii wa Bongo Movie, Wema Sepetu hajafikishwa mahakamani Kisutu leo kwa madai kuwa amepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali leo kwa ajili ya kupimwa na kuthibitisha iwapo anatumia madawa ya kulevya au la!
Imedaiwa kuwa, Polisi Dar, wamefikia hatua hiyo baada Wema kukana kutumia madawa wakati alipokuwa akihojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi.
Taarifa zimedai kuwa mastaa wenzake kama TID na wengine walikiri kutumia madawa na kupewa onyo kali huku mahakama ikiwapa masharti matatu likiwemo la kuripoti polisi mara mbili kwa mwezi ndani ya mwaka mmoja na kuwa chini ya uangalizi wa mahakama, kisha kujidhamini kwa bondi ya shilingi milioni moja na kurudi uraiani wakati Wema akikana kutumia madawa.
Taarifa zaidi zimedai kuwa, polisi wanaendelea kumshikilia Wema huku wakisubiri ripoti ya mkemia mkuu ili waweze kukamilisha upelezi na kumchukulia hatua zinazostahili.
Wednesday, February 8, 2017
Wema Sepetu Apelekwa Kupimwa Kwa Mkemia Mkuu wa Serikali Kujua Kama Anatumia Madaw Au Lah.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
New Posts
Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko
Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...
-
.Na.Ahmad Mmow. Mahakama ya mkoa wa Lindi,leo imewachia huru makada watatu wa CHADEMA waliokuwa wanakabiliwa na shitaka la kushiwishi kute...
-
KINGS FM TOP 30 MAY 27 KWA NGWARU BADO NI SHEEEDAH Midundo mikali inasikika kila kona kwenye media tofauti tofauti duniani kote, Nchin...
-
1. Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amezungumzia sababu za kukosekana kwa hotuba yake Bungeni na kusema Wame...
No comments:
Post a Comment