Msanii Lameck Ditto ambaye sasa anafanya vyema na wimbo wake 'Moyo sikuma damu' amefunguka na kusema yeye hausiki na biashara ya dawa za kulevya wala matumizi ya dawa za kulevya na kusema kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaama amekosea kutaja jina.
Lameck Ditto akiongea na EATV amesema kuwa hata yeye amesikia jina lake likitajwa kwenye kundi la wasanii ambao wanahitajika kufika kesho kituo cha polisi na kusema anadhani kuwa Mkuu wa Mkoa alikosea kutaja jina lake.
"Kiukweli mimi mwenyewe nimeshtuka sana maana sijihusishi kwa namna yoyote na madawa ya kulevya, siuzi wala kutumia na siku zote nayapiga vita sababu natambua si mazuri katika jamii, nadhani Mhe. alikosea kutaja jina maana alisema Ditto lakini baadaye niliona amerekebisha na kusema Titto, hivyo naomba Watanzania watambue mimi sihusiki na madawa ya kulevya" alisema Lameck Ditto
Thursday, February 2, 2017
Sihusiki na madawa ya kulevya - Ditto
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
New Posts
Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko
Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...
-
.Na.Ahmad Mmow. Mahakama ya mkoa wa Lindi,leo imewachia huru makada watatu wa CHADEMA waliokuwa wanakabiliwa na shitaka la kushiwishi kute...
-
KINGS FM TOP 30 MAY 27 KWA NGWARU BADO NI SHEEEDAH Midundo mikali inasikika kila kona kwenye media tofauti tofauti duniani kote, Nchin...
-
1. Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amezungumzia sababu za kukosekana kwa hotuba yake Bungeni na kusema Wame...
No comments:
Post a Comment