Monday, September 18, 2023

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

 


Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbwa na mafuriko makubwa ya mashariki mwa nchi hiyo.


Jumapili iliyopita, kimbunga cha “Daniel” kilipiga maeneo kadhaa mashariki mwa Libya, na hasa hasa miji ya Benghazi, Al-Bayda, Marj, Susa, Shahatt na Derna.


Baada ya kimbunga hicho, Shirika la Afya Duniani lilionya kuhusu kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokumbwa na kimbunga na mafuriko hayo.


Kwa mujibu wa shirika la habari la IRIB, Haidar al-Sayeh, mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Magonjwa nchini Libya, alitoa taarifa na kutangaza idadi ya sumu ambazo zimeripotiwa kutokana na matumizi ya maji ya kunywa huko Derna, Libya.


Akizungumzia kutotumika maji ya kunywa katika jiji la Derna, Al-Sayeh amesema kuwa, hali ya hatari ya mwaka mmoja itatangazwa katika maeneo yaliyoathiriwa na dhoruba na mafuriko mashariki mwa Libya ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa wowote wa kuambukiza katika maeneo haya.


Shirika la Afya Duniani lilitangaza siku ya Jumamosi kuwa, zaidi ya watu 9,000 wametoweka katika mji wa Derna mashariki mwa Libya.


Idadi ya waliofariki kutokana na kimbunga hicho nchini Libya hadi sasa imetangazwa kuwa zaidi ya 11,000.

No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...