Tuesday, January 31, 2017

Shule 6 Dar hoi matokeo kidato cha nne


WAKATI Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) likitangaza matokeo ya Kidato cha Nne kwa mwaka 2016 na kuonesha ufaulu wa jumla kwa watahiniwa wa shule umeongezeka kwa asilimia 2.44, idadi ya watahiniwa waliopata alama za kuwawezesha kuendelea na kidato cha tano imekuwa chini kwa miaka mitatu mfululizo.

Matokeo ya mtihani uliofanyika Novemba, 2016 na kutangazwa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk Charles Msonde, yanaonesha watahiniwa wa shule 244,762 ambayo ni asilimia 70.35 ya waliofanya mtihani walifaulu mtihani huo.

Ufaulu huo unaonesha kuongezeka kwa asilimia 2.44 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2015 ambayo wanafunzi 240,996 ambao ni asilimia 67.91 walifaulu na kwa mwaka 2014 walikuwa ni 169,642 (asilimia 69.76) na mwaka 2013 walikuwa ni 201,152 ambao ni asilimia 57.09.

Jumla ya watahiniwa 408,372 walisajiliwa kufanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2016, wakiwemo wasichana 209, 456 sawa na asilimia 51.29 na wavulana 1998, 916 (asilimia 48.71).

Kati yao wote waliosajiliwa, watahiniwa wa shule walikuwa 355,822 na wa watahiniwa wa kujitegemea walikuwa 52,550. Ufaulu kwenda Kidato cha V Pamoja na ufaulu huo kuongezeka, inaonesha kuwa watahiniwa wanaopata madaraja yanayoweza kuwafanya wakaingia kidato cha tano (daraja la I-III), inaonekana kuwa chini ya asilimia 50.

Kwa matokeo ya mwaka jana, watahiniwa 96.018 ambao ni asilimia 27.60 wamepata daraka la I-III, wakati mwaka 2015 walikuwa ni 89,929 ambayo ni asilimia 25.34 na mwaka 2014 walikuwa ni 73,832 ambao ni asilimia 30.72.

Watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu mtihani ni 32,521 sawa na asilimia 68.19. mwaka 2015 walikuwa ni 31,1951 sawa na asilimia 64.80, hivyo ufaulu kuongezeka kwa asilimia 3.39. Kwa upande wa maarifa, watahiniwa 8,751 sawa na asilimia 50.48 wamefaulu, mwaka 2015 watahiniwa 7,536 ambao ni asilimia 46.63 hivyo kuwapo ongezeko ya ufaulu kwa asilimia 3.85.

Kuhusu ufaulu wa masomo unaonesha kuwa masomo ya Historia, Jiografia, Kiswahili, Kiingereza, Hisabati, Fizikia, Biolojia, Commerce na Book-Keeping umepanda kwa asilimia 0.12 na asilimia 8.08 ikilinganishwa na mwaka 2015.

Watahiniwa wanaonekana kufanya vizuri zaidi kwenye somo la Kiswahili ambapo ufaulu wake ni asilimia 77.75 ya watahiniwa wote, ingawa ufaulu huo umeonekana kushuka ukilinganisha na mwaka 2015 uliokuwa ni asilimia 77.63 na mwaka 2014 ulikuwa asilimia 69.66.

Aidha, watahiniwa wameshindwa kufanya vizuri katika somo la Hisabati ambalo pamoja na kuonekana ufaulu umeongezeka waliofaulu somo hilo ni asilimia 18.12 ya watahiniwa wote wa shule, mwaka 2015 walikuwa ni asilimia 16.76 na mwaka 2014 ilikuwa ni asilimia 19.58.

“Pamoja na asilimia ya ufaulu wa jumla kuendelea kuimarika, takwimu zinaonesha kuwa bado ufaulu wa masomo na watahiniwa waliopata daraja la I-III ni chini ya asilimia 50, hivyo juhudi za makusudi zinahitajia kuendelea kufanya ili kuinua kiwango cha ufaulu wa masomo na kuongezeka kwa idadi ya watahiniwa kwenye madaraja ya ufaulu,” alisema Dk Msonde.

Shule za binafsi vinara
Kuhusu upangaji wa matokeo kwa shule zenye wanafunzi zaidi ya 40, unaonesha shule za watu binafsi na mashirika ya dini zimeendelea kufanya vizuri katika nafasi za 10 bora kitaifa huku zile zinazomilikiwa serikali zikiendelea kufanya vibaya kwa miaka mitatu mfululizo.

Shule 10 Bora ni Feza Boys (Dar es Salaam), St Francis Girls (Mbeya), Kaizirege Junior (Kagera), Marian Girls, Marian Boys na St Aloysius Girls (Pwani), Shamsiye Boys (Dar es Salaam), Anwarite Girls (Kilimanjaro), Kifungilo Girls (Tanga) na Thomas More Machrina (Dar es Salaam).

Aidha, Mkoa wa Dar es Salaam umezorota kielimu baada ya kuwa na shule sita kati ya 10 zilizoshika nafasi za mwisho. Shule hizo ni Kitonga na Nyeburu (Dar es Salaam), Masaki (Pwani), Mbopo, Mbondole na Somangila Day (Dar es Salaam), Dahani (Kilimanjaro), Ruponda (Lindi), Makiba (Arusha) na Kidete (Dar es Salaam).

Mikoa iliyofanya vizuri katika nafasi ya 10 bora ni Njombe, Iringa, Kagera, Kigoma, Kilimanjaro, Mwanza, Pwani, Ruvuma, Shinyanga, Tabora wakati halmashauri 10 bora ni Bukoba Mjini, Njombe Mjini, Kakonko, Kahama Mji, Wanging’ombe, Ilemela, Iringa Mjini, Mkuranga, Igunga na Kibaha Mji.

Ufaulu kwa watahiniwa 10 bora waliofanya vizuri kitaifa unaonesha kuwa ni asilimia 50-50 kwa wavulana na wasichana huku mwaka 2016 wakiongozwa na mvulana. Mwaka 2015, watahiniwa wa kike walikuwa ni wanne na wavulana sita na mwaka 2014 walikuwa na uwiano sawa, lakini waliongozwa na mwanafunzi wa kike.

Mvulana aongoza, msichana achomoza
Kwa 2016, watahiniwa 10 bora ni Alfred Shauri (Feza Boys), Cynthia Mchechu (St Francis Girls), Erick Mamuya (Marian Boys), Jigna Chavda (St Mary Goreti), Naomi Tundui (Mariam Girls), Victoria Chang’a (St Francis Girls), Brian Johnson (Marian Boys), Esther Mndeme (St Mary’s Mazinde Juu), Ally Koti (ALCP Kilasara) na Emmanuel Kajege (Marian Boys).

Watahiniwa wasichana 10 bora ni Cynthia, Jigna, Naomi, Victoria, Esther, Christa Edward (St Francis Girls), Nelda John (Marian Girls), Mariana Shabani (Kifungilo Girls), Beatrice Mwella (St Mary’s Mazinde Juu) na Rachel Kisasa (Canossa).

Wavulana 10 bora kitaifa ni Alfred, Erick, Brian, Ally, Emmanuel, John Ng’hwaya (Nyegezi Seminary), Clever Yohana (Livingstone Boys Seminary), Desderius Rugabandana (Morning Star), Kennedy Boniface na Assad Msangi (Feza Boys).

126 wafutiwa, 40 matokeo yazuiwa
Katika hatua nyingine, Dk Msonde alisema Necta limezuia matokeo ya watahiniwa 33 waliopata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mitihani katika baadhi ya masomo, pia matokeo ya watahiniwa 124 waliopata matatizo ya kiafya na kufanya masomo yote, watahiniwa wamepewa fursa ya kufanya mitihani wa Kidato cha Nne 2017.

Alisema pia baraza limezuia matokeo ya wanafunzi 40 wa Shule ya Sekondari ya Hellens wanaodaiwa alama endelevu hadi hapo mkuu wa shule atakapowasilisha alama hizo huku likifuta matokeo ya watahiniwa 126 waliobainika kufanya udanganyifu akiwamo mmoja aliyeandika matusi katika karatasi ya majibu.

Kati ya waliofutiwa matokeo 58 ni wa kujitegemea na 58 ni wa shule, 10 watihani wa maarifa. Mvulana kinara anena Akizungumza na gazeti hili, mwanafunzi bora kitaifa, Alfred Shauri alisema siri ya mafanikio yake ni bidii na kumtanguliza Mungu.

Alfred ambaye pia amefanya vizuri kwenye insha ya Afrika Mashariki alisema: “Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kufikia ndoto yangu ya kufanya vizuri na nitaendelea kufanya bidii kwenye masomo, ingawa kufanya vizuri kidato cha nne haikupi njia ya kufanya vizuri kwenye mitihani ya elimu ya juu kama hujitumi.”

Kijana huyo ambaye ni mtoto wa tatu katika familia ya watoto wanne, anasema pamoja na wazazi wake kumtaka kufanya masomo ya sayansi ili kuwa mhandisi, ingawa anapenda fani hiyo, lakini angependa kujikita zaidi katika kuwekeza kwenye biashara na ujasiriamali. Mama yake Alfred, Adela Shauri pamoja na kumpongeza mwanawe, alisema mtoto wake ni kijana mwenye upendo na huruma ambaye anapenda kujibidisha kwenye masomo au kwa kile anachikifanya.

“Yaani mpaka nimetetemeka niliposikia haya matokeo, lakini niseme ni mtoto mwenye bidii katika masomo na anayemtangulia Mungu katika kila jambo. Niwaombe wazazi wenzangu kuhakikisha tunawalea watoto wetu wakiwa na hofu ya Mungu, kwani peke yetu hatutaweza,” alisema.

Kwa upande wa mwanafunzi aliyeshika nafasi ya pili kitaifa na akiwa ni mwanafunzi bora kwa upande wa wasichana, Cynthia Mchechu alisema: “Mpaka sasa siamini haya matokeo, natamani kama nikalale hivi. Lakini nashukuru sana Mungu, kwani bidii katika masomo ndiyo imemfanya kufikia hapo.”

Msichana bora haamini
Cynthia anawashauri wanafunzi wenzake kuhakikisha wanatimiza ndoto zao kwa kujibidiisha na kuhakikisha wanakamilisha kile wanachotaka kupata katika maisha.

Naye Mercy Mchechu, mama mzazi wa Cynthia ambaye ni mtoto pekee wa kike kwake na mumewe Nehemia Mchechu, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), anasema mwanawe amekuwa na juhudi ya masomo tangu akiwa anasoma shule ya awali na msingi Rightway ya Dar es Salaam ambayo yeye ndiye mkurugenzi wake.

“Ni binti ambaye ana bidii katika masomo na ana uwezo wa kutambua kile anachokitaka maishani na akaweza kutekeleza,” alisema Mercy.

Magazeti ya Tanzania February 1, 2017 kuanzia, Udaku, Hardnews na michezo

February 1, 2017

Tarehe / siku nzuri kwa mimba kuweza kutungwa

Leo napenda nizungumzie jambo moja tu ambalo ni juu ya  jambo moja tu, nalo ni namna wanavyoweza kui-pin point siku ile ya kilele (i.e fruitful/productive/fertile day), hapa nina maana ya siku ile ambayo wao wanaiita siku ya 14. 

Ikumbukwe kuwa wanawake wanatofautiana katika suala zima la urefu wa MENSTRAL CYCLE, yaani idadi ya siku kati ya period ya kwanza hadi ile ya pili inayofuatia. Kundi kubwa la wanawake wana fall kwenye range ya siku 22-35. Japo walio-normal wana siku 28. Vile vile kuna wengine huwa na menstral cycle mbili, yaani fupi na ndefu. Hivyo walio na menstral cycle fupi, mathalani wale wenye siku 22, huwa vilevile wana kipindi kifupi sana cha kutokwa na damu (period), yaani damu inaweza kukatika ndani ya siku 2 tu! Na wale wenye siku 35 au zaidi huwa wana kipindi kirefu sana cha kutokwa na damu (period) ambapo wengine huwachukua hata siku kati ya 5 hadi 8. 

Hivo basi, kama wewe ni mwanaume inakubidi umwelewe vizuri mwenzi wako juu ya hayo niliyoyasema hapo juu ili ikusaidie kui-pin point ile fertile day (yaani siku ya mimba). 

Swali: Je siku ya mimba ni ipi? 
Jibu lisilosahihi: Watu wengi na hata baadhi ya wanasayansi wanafikiri siku ya mimba ni ile ya 14 baada  ya dalili za kwanza za damu ya hedhi! Wao huhesabu kuanzia siku ile damu ilipoanza kutoka hadi siku ya 14! Utaratibu huu ume-prove failure! Hii ni kwa sababu wanawake wana menstral cycle
zinazotofautiana kwa urefu. Hivo basi jibu sahihi ni hili hapa chini:

Jibu sahihi:  
1. Kwanza inabidi ujue kama mwenzi wako ana menstral cycle ipi? Fupi au ndefu, ama zote mbili?

2. Baada ya kujua urefu wa menstral cycle ya mwenzi wako then pin point siku ile ya mwisho halafu
uhesabu backwards siku 15 kuanzia siku ile ya mwisho. Siku hii ya 15 kuanzia mwisho ndiyo siku ya  mimba kwa mwanamke yeyote! 

Once you know the '15th day' from the last one, then you can manoeuvre whatever you want to get her pregnant or to avoid pregnancy! 

With this new approach of pin pointing the fertile day you will find that all women (menstral cycles)
are covered, whereas the old way of counting fits only to women whose menstral cycles are 28 days!

Naomba nitoe mifano hai kwa faida ya dada zetu na wengine: 
1. Kama mwanamke ana menstration cycle ya siku 22 inabidi afanye kama ifuatavo: Kwanza
itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama hapa
chini:

1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th,
20th, 21st, 22nd.

Kisha ahesabu kuanzia ile 22nd day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15. Ataona kuwa siku ya
kumi na tano inaangukia kwenye 8th day ya kalenda yake. Hivo 8th day ndiyo siku ya mimba
kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 22. Akumbuke kwamba 1st day
ndiyo siku anayoanza ku-bleed!

2. Kama mwanamke ana menstration cycle ya siku 28 inabidi afanye kama ifuatavo: Kwanza
itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama hapa
chini: 

1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th,
20th, 21st, 22nd, 23rd, 24th, 25th, 26th, 27th, 28th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 28th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15. Ataona kuwa siku ya
kumi na tano inaangukia kwenye 14th day. Inamaana kwamba 14th day ndiyo siku ya mimba
kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 28. Akumbuke kwamba 1st day
ndiyo siku anayoanza ku-bleed!

3. Kama mwanamke ana menstration cycle ya siku 35 inabidi afanye kama ifuatavo: Kwanza
itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama hapa
chini: 

1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th, 16th, 17th, 18th, 19th,
20th, 21st, 22nd, 23rd, 24th, 25th, 26th, 27th, 28th, 29th, 30th, 31st, 32nd, 33rd, 34th, 35th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 28th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15. Ataona kuwa siku ya
kumi na tano inaangukia kwenye 21st day. Inamaana kwamba 21st day ndiyo siku ya mimba kwa
mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 35. Akumbuke kwamba 1st day ndiyo
siku anayoanza ku-bleed!

4. Kama mwanamke ana abnormal menstration cycle ya siku 15 , BASI KUNAUWEZEKANO
WA KUTOPATA MIMBA KABISA KAMA INAVYOONEKANA HAPA CHINI: 

Kwanza itabidi atengeneze kalenda yake mwenyewe ya siku zake zote za menstration cycle kama
kawaida: 

1st, 2nd, 3rd, 4th, 5th, 6th, 7th, 8th, 9th, 10th, 11th, 12th, 13th, 14th, 15th.

Kisha ahesabu kuanzia ile 15th day kurudi nyuma mpaka afikishe siku 15. Ataona kuwa siku ya
kumi na tano inaangukia kwenye 1st day. Inamaana kwamba, the 1st day of her bleedind ndiyo
siku ya mimba kwa mwanamke yeyote ambaye ana menstration cycle ya siku 15. Akumbuke
kwamba 1st day ndiyo siku anayoanza ku-bleed, na ndiyo hiyo hiyo siku ambayo mwanamke wa
kundi hili anaweza kupata mimba!

Hii inamaana kwamba, siku ambayo linaharibika lile yai la upande mmoja ndiyo siku hiyo hiyo
ambayo yai la upande wa pili linapevuka tayari kwa kurutubishwa. Mwanamke wa aina hii
anaweza kupata mimba tu kama atakutana na mwanaume siku ile anayoanza kubleed, kwani siku
ambayo yai moja linaanza kuharibika ndio siku hiyo hiyo ambayo yai la upande wa pili
linakuwa tayari kurutubishwa!

Na wanawake wa kundi hili la nne ukiwauliza vizuri watakiri kwamba hawajawahi kuona au ku-feel ule ute mweupe ambao wenzao huwa wanaupata siku ile yai linapokuwa tayari kwa
kurutubishwa, kwani ute wa wanawake wa kundi hili la nne huwa unachanganyikana na damu
kwa vile unatoka siku ile ile wanapoanza ku-bleed. Pia wanawake wa kundi hili huwa
wanatokwa na kiasi kidogo sana cha damu; na bleed hukatika ndani ya siku moja au mbili tu! 

Jambo la kushangaza ni kwamba, wanawake wengi hawana knowledge ya kutosha juu ya hili
suala la siku ya mimba; hasa wale ambao wana menstration cycle inayobadilikabadilika! Wao
husitukia tu wameanza ku-bleed. Ndo maana hawawezi hata ku-plan kutopata mimba! Hawana
ujanja kabisa ndio sababu wengi wanatumia sindano na njia zingine nyingi za artificial ambazo
mwisho wa siku huwaletea matatizo ya uzazi, kwani nyingi hu-block njia ya uzazi! Nimeona
wengi wenye matatizo ya uzazi unaosababishwa na hizi artificial family planning. Wengine
hulazimika kwenda hospital kuzibuliwa ili wapate mimba jambo ambalo ni hatari kwa afya zao!
Full maelezo ya kujitosheleza, ukikosa kudaka au kudakisha mimba basi kuna walakini...

Matokeo ya Kidato cha nne 2016 Luhololo Secondary

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2016 EXAMINATION RESULTS

S2056 LUHOLOLO SECONDARY SCHOOL

DIV-I = 0; DIV-II = 3; DIV-III = 5; DIV-IV = 30; DIV-0 = 2

CNO

SEX

AGGT

DIV

DETAILED SUBJECTS

S2056/0001

F

30

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0002

F

35

0

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0003

F

23

III

CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B' PHY - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'C' B/MATH - 'D'

S2056/0004

F

23

III

CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'F'

S2056/0005

F

30

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0006

F

33

IV

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0007

F

32

IV

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0008

F

33

IV

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0009

F

30

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0010

F

32

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0011

F

33

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0012

F

33

IV

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0013

F

33

IV

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0014

F

26

IV

CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'D' BIO - 'D' B/MATH - 'D'

S2056/0015

F

33

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0016

F

30

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0017

F

30

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0018

F

31

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0019

F

32

IV

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0020

M

29

IV

CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0021

M

31

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0022

M

21

II

CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'D'

S2056/0023

M

35

0

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'F' ENGL - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0024

M

31

IV

CIV - 'F' HIST - 'F' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'D'

S2056/0025

M

29

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0026

M

24

III

CIV - 'D' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'D'

S2056/0027

M

31

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0028

M

20

II

CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B' PHY - 'D' CHEM - 'C' BIO - 'C' B/MATH - 'D'

S2056/0029

M

29

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0030

M

30

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0031

M

29

IV

CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'F' KISW - 'D' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0032

M

31

IV

CIV - 'D' HIST - 'F' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'F' B/MATH - 'F'

S2056/0033

M

27

IV

CIV - 'D' HIST - 'C' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0034

M

28

IV

CIV - 'F' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0035

M

24

III

CIV - 'D' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'C' B/MATH - 'F'

S2056/0036

M

27

IV

CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'D' PHY - 'F' CHEM - 'F' BIO - 'C' B/MATH - 'F'

S2056/0037

M

27

IV

CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

S2056/0038

M

24

III

CIV - 'C' HIST - 'D' GEO - 'C' KISW - 'D' ENGL - 'C' PHY - 'D' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'D'

S2056/0039

M

21

II

CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'B' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'F'

S2056/0040

M

29

IV

CIV - 'D' HIST - 'D' GEO - 'D' KISW - 'D' ENGL - 'D' CHEM - 'F' BIO - 'D' B/MATH - 'F'

Giggy Money: Mabwana wa Wema Wananishobokea Wenyewe

Kufuatia kusambaa kwa video yake akifanya vitendo vya kifuska hadharani na aliyekuwa mpenzi wa staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu, Ibrahim Mgimbu ‘Calisah’ mwanadada anayeuza nyago kwenye video za Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ amefunguka na kusema wenyewe ndiyo wanaomshobokea.

 Video hiyo chafu ya Gigy na Calisah ilisambaa hivi karibuni kwenye mitandao ya kijamii ambapo watu wengi walionekana kumshangaa mwanadada huyo huku wakimtolea maneno ya kejeli kuwa hajatulia na amekuwa akipenda kuwa kimapenzi na wanaume waliopitia kwa Wema akiwemo Idris Sultan. Baadhi ya mashabiki waliozungumza na Wikienda walifunguka kuwa, Gigy anatakiwa kubadilika kwani amekuwa mtu wa matukio kila siku na amekuwa akipita kule alikopita Wema kwa sababu alianza na Idris na sasa Calisah.

“Hivi Gigy haoni wanaume wengine hadi ajibebishe kwa wale ambao tayari walishakuwa na uhusiano na Wema? Hata sielewi Gigy anajisikiaje maana hii video yake na wanafanya vitendo vya kimahaba huku akiwa ana uhusiano na mpenzi wake wa siku zote Moj (Mourald Alpha) sijui naye huwa anaonaje na anajisikiaje anapoona mwanamke wake anafanya hivyo,” alisema shabiki mmoja aliyezungumza na Wikienda.

Baada ya kuvutiwa waya na kuulizwa kulikoni kupenda kupita alikopita Wema na kujirekodi video za kimahaba na kuziachia mitandaoni, Gigy alikuwa na haya ya kusema:
“Kwanza niseme hiyo video siku hiyo, Calisah ndiye aliyenishobokea maana ndiye aliyenifuata, kuhusu wanaume aliotoka nao Wema ni kwa sababu labda nyota yangu inamzidi maana wenyewe ndiyo wamekuwa wakinifuata kwa kifupi wanaume wa Wema ndiyo huwa wananishobokea. “Kuhusu Moj, ni mpenzi wangu na ni mume wangu mtarajiwa na ni baba wa mwanangu maana nina ujauzito wake.”

Linah awataja wanaomnyima usingizi kwenye muziki wa bongo fleva

Msanii Linah Sanga amefunguka na kuwataja wasanii ambao wanamyima usingizi na kusema hao ndiyo washindani wake kwenye muziki wa bongo fleva kwa sasa.

Linah Sanga alisema hayo kupitia kipindi cha 'Ngaz kwa Ngaz' na kudai kuwa licha ya muziki wa bongo fleva kuwa na idadi kubwa ya wasanii wa kike sasa tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma haimuumizi ila anapata changamoto ambazo zinamfanya aumize kichwa na kukosa usingizi kutafuta kitu kipya cha kipekee.

"Kwa sasa hivi naweza kusema mshindani wangu mkubwa ni wasichana wote ambao saizi wanafanya vizuri mfano Ruby, Maua, Vanessa kwa sababu wote wamekuja na tunafanya muziki ambao upo sawa, lakini mimi hainiumizi ila inanifanya nizidi kujiuliza kila siku silali, natafuta kitu cha tofauti ili niwe tofauti na Maua, nifanye nini niwe tofauti na Vanessa na nifanye nini ili niwe tofauti na Rubby" alisema Linah Sanga

Monday, January 30, 2017

Waliookolewa mgodini watoka hospitali


Geita. Wachimbaji 15 waliokuwa wamelazwa katika hospitali ya Mkoa wa Geita kwa ajili ya matibabu baada ya kuokolewa katika mgodi wa RZ walikokuwa wamefunikwa na kifusi cha udongo kwa siku tano wameruhusiwa kutoka hospitali baada ya afya zao kuwa nzuri.

Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Brian Mawala amesema afya za wachimbaji hao zimeimarika na wana uwezo wa kuendelea na kazi.

Baada ya kuruhusiwa leo asubuhi wamekutana na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga.

Belle 9: Baba na mama yangu ndio couple ninayoikubali zaidi

Ni couple gani ambayo unailewa zaidi hapa Bongo? Ni swali ambalo mtangazaji wa kipindi cha The Playlist cha Times FM, Lil Ommy alimuuliza Belle 9.

“Baba yangu na mama yangu,” alijibu muimbaji huyo.

“Wananivutia kwasababu nyumbani maisha ni ya kawaida lakini still baba yuko na mama halafu mara zote ambazo nimekuwa nyumbani, sijawahi kuona mama yangu anagombana na baba. Mimi nimekaa sana nyumbani kwa muda mrefu, lakini mara ya kwanza naona kama wanashikanashikana hivi ilikuwa mimi ndio chanzo, yaani mama alikuwa ananitetea mimi kwasababu baba alikuwa ananinyoosha sana sasa mama alikuwa kama anaingia hivi, lakini haukuwa ugomvi,” ameongeza.

“Kiukwezi ni best couple kwangu mimi, najifunza mengi kupitia pale, inanipa nguvu nikirudi nyumbani baba yupo, mama yupo nikitoka hapo nami nakuwa nipo fast kila kitu.”

Kwa upande wa couple ambayo haielewi ni ile ya Kanye West na Kim Kardashian.

Umeuona mjengo anaojenga Diva?


Diva The Bawse sio mtu wa mchezo mchezo, amewaonesha mashabiki jambo ambalo limewashtua katika mtandao wa Instagram.

Mtangazaji huyo wa kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM, amepost picha katika mtandao huo ya mjengo wake anaodai anaujenga huku akiweka wazi kuwa utakamilika ifikapo mwaka 2018.

“Tusichukuliane POA ila nene Hard work Pays Aisee, don giv Up guys !. focus and Msidharau Online ads , Haya Matangazo ya Insta By 2018 yatamaliza Hii nyumba yangu. Tuseme Inshaallah 💞,” ameandika Diva katika picha ya nyumba hiyo.

Endapo nyumba hiyo itakamilika itamfanya mtangazaji huyo kuwa miongoni mwa mastaa wenye mijengo mikali hapa Bongo.

BREAKING NEWS: Mwenyekiti wa CCM Mbeya anusurika kuuawa kwa Risasi

Mwenyekiti wa CCM Mbeya Mjini, Efrahim Mwaitenda mwenye umri wa miaka 60 amejeruhiwa kwa kupigwa risasi mgongoni na mtu au watu wasiofahamika.

 

Mwenyekiti wa CCM Mbeya Mjini (Aliyekaa) akipeleka hospitali)

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Emmanuel Lukula amesema tukio hilo limetokea mnamo tarehe 29.01.2017 majira ya saa 05:45 usiku katika kitongoji cha Ilopa, Kijiji cha Mahenge, Kata ya Makwale, Tarafa ya Ntebela, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya.

Amesema tukio hilo limetokea wakati akiwa amelala kitandani nyumbani kwake Ntembela ambapo mbinu iliyotumika ilikuwa ni  kukata wavu wa dirisha na kumjeruhi kwa kutumia silaha za kienyeji zinazotumia risasi za gololi.

Mwenyekiti huyo amefikishwa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na hali yake inaendelea vizuri.

Lukula amewaambia waandishi wa habari kuwa nia ya shambulizi hilo ilikuwa ni kutaka kuumua na kwamba juhudi za kuwatafuta na kuwakamata wahusika zinaendelea 

TFF yaguswa na Kifo cha mchezaji wa Kagera Sugar

 Shirikisho la Kandanda nchini Tanzania TFF limesema kuwa limepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha David Burhan mchezaji wa Kagera Sugar ambaye mefariki usiku wa kuamkia leo.

Kupitia ukurasa wake wa twitter rais wa shirikisho ls soka Jamal Malizi aliandika haya "Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha David Abdalah Burhan mchezaji wa Kagera Sugar.Amefariki usiku wa kuamkia leo.Apumzike kwa amani.alisema Malizi.

Mapema hibvi leo taarifa za msiba wa Kipa wa Kagera Sugar, David Burhani zilianza kuvuma haswa kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii kwamba amefariki dunia.

David Buruhan kipa wa Kagera Sugar na mtoto wa Mshambuliaji wa zamani wa PAN Abdallah Buruhan amefariki katika Hospital ya Bugando jijini Mwanza alikokuwa amelazwa baada ya kusumbuliwa na Malaria, Burhani aliwahi kuichezea Mbeya City na baadaye aliweza kujiunga na Majimaji ya Songea na kuitumikia msimu mmoja.

Taarifa zaidi endelea kufuatilia taarifa zetu.




Picha: Meli kubwa ya kisasa ya Azam yatia nanga Bandari ya Tanga kwa mara ya kwanza


 Meli mpya na ya kisasa iitwayo AZAM SEALINK 2 aina ya RORO yenye uwezo wa kubeba abiria wapatao 1650, mizigo uzito wa tani 717 sambamba na magari 150 imetia nanga
Bandari ya Tanga leo.

Meli hiyo inatarajiwa kufanya safari zake na kutoa huduma za kubeba abiria na mizigo ikiwemo magari kutoka Pemba kwenda Unguja hadi Tanga mara moja kwa wiki.








New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...