Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka manne ya uchochezi.
Lissu amepandishwa kizimbani saa 6:25 na kusomewa mashtaka hayo na Wakili wa Serikali Kishenyi Mutalemwa.
Mutalemwa amesema upelelezi wa kesi hiyo bado lakini akawasilisha maombi ya kupinga dhamana ya mshtakiwa.
Katika maombi hayo amesema mshtakiwa Lissu anakabiliwa na kesi nyingine tatu mahakamani hapo na kwamba ingawa yuko nje kwa dhamana lakini amekuwa na mwenendo unaohatarisha amani si tu kwa wanajamii, bali hata kwake mwenyewe kwa kuendelea kutoa maneno ya uchochezi.
Hata hivyo maombi hayo yalipingwa na Wakili wa Lissu Peter Kibatala akisema kuwa mashtaka yake yanadhaminika.
Amesema kiapo cha kupinga dhamana kilichotolewa na mkuu wa upelelezi wilaya ya Ilala, ASP Denis Mjumba kina dosari za kisheria kwani hakikidhi masharti ya viapo.
Mabishano bado yanaendelea, Wakili Kibatala bado anatoa hoja kabla ya Hakimu Huruma Shaidi kutoa uamuzi.
Thursday, February 9, 2017
Tundu Lissu Kapandishwa Kizimbani LEO na Kusomewa Mashitaka Manne ya Uchochezi
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
New Posts
Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko
Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...
-
.Na.Ahmad Mmow. Mahakama ya mkoa wa Lindi,leo imewachia huru makada watatu wa CHADEMA waliokuwa wanakabiliwa na shitaka la kushiwishi kute...
-
KINGS FM TOP 30 MAY 27 KWA NGWARU BADO NI SHEEEDAH Midundo mikali inasikika kila kona kwenye media tofauti tofauti duniani kote, Nchin...
-
1. Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amezungumzia sababu za kukosekana kwa hotuba yake Bungeni na kusema Wame...
No comments:
Post a Comment