Thursday, April 5, 2018

ZILIZOBAMBA



1. Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amezungumzia sababu za kukosekana kwa hotuba yake Bungeni na kusema Wamegomea Kusoma Hotuba Za Kambi Hiyo Kwa Wizara Yoyote Mpaka Watumishi Wa Ofisi Hiyo Watakaporejeshwa Kazini.
Freeman Mbowe

2. Moja kati ya stori inayoshika headlines kutoka nchini Libya ni hii kutoka Mahakama ya Tripoli ambayo imefuta kesi ya mauaji iliyokua ikimkabili Saadi Gaddafi, mtoto wa tatu wa aliekua rais wa Libya, Muammar Gaddafi.

Saadi Kaddafi amefutiwa mashtaka yote dhidi yake katika kesi ya mwanamichezo Bachir al-Rayani ambaye alifariki dunia mwaka 2006 baada ya kupigwa kichwani, Bachir Rayani alifariki dunia baada ya malumbano katika nyumba inayomilikiwa na Saadi Gaddafi.

3. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kutoa uamuzi April 23,2018 kuhusu kesi ya kutumia dawa za kulevya inayomkabili mrembo Wema Sepetu na wenzake kama wana kesi ya kujibu au hapana na uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi watano wa upande wa mashtaka.

Mbali na Wema washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya kutumia dawa za kulevya ni Angelina Msigwa  na Matrida Seleman Abbas.
Wema Sepetu


4. wasanii wengi kutoka Zanzibar wamekuwa waisahau fadhila na kusahau walikotoka hasa pale wanapohamishia majukumu yao kikazi Jijini Dar es Salaam, huyu hapa ni nedy music kutoka Zanzibar hapa anawajibu mashabiki wake ambao wanasema amekusahau kabisa Zanzibar.
Nedy Music

5. Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara amewataka Watanzania wawe wepesi wa kutoa pongezi pale wasanii wa filamu nchini Tanzania wanapofanya vizuri, na sio kuwabeza na kuwaponda kila siku kwani kitendo hicho kinawakatisha tamaa waigizaji wetu.
Haji Manara

Via ➡KingsFmRadio 104.3Mhz
      ➡KingsFmRadioAndroidApp 
      ➡Tunnein 12:00-12:15 pm
         www.kingsfm.co.tz

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...