Thursday, January 5, 2017

Marekani kubaini lengo la udukuzi wa Putin katika uchaguzi


Mkurugenzi wa vitengo vya ujasusi nchini Marekani James Clapper amesema kwamba Marekani haijapata changamoto kubwa ya kuingiliwa uchaguzi wake zaidi ya vitendo vya Urusi katika uchaguzi huo wa urais.

Bwana Clapper alikuwa akizungumza wakati wa uzinduzi wa uchunguzi wa maseneta wa Marekani kuhusu uhalifu wa mtandaoni kabla ya uchaguzi huo.

Ameonya kuwa uhalifu wa mtandaoni unaotekelezwa na Urusi ni tishio kubwa kwa serikali ya Marekani ,lakini udukuzi wa Urusi haukubadilisha jumla ya kura.

Rais mtule Donald Trump alikuwa ametilia shaka hatua ya Urusi kuingilia uchaguzi huo, lakini katika ujumbe wake wa Twitter siku ya Alhamisi alisisitiza kuwa mfuasi mkubwa wa vitengo vya ujasusi nchini Marekani.

Mwenyekiti wa kamati ya huduma za ulinzi, John McCain alisema kuwa lengo la uchunguzi huo halikuwa kutilia shaka matokeo ya uchaguzi.

No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...