Monday, September 18, 2023

Taiwan yanasa ndege 103 za kivita za China kwenye anga yake



 Wizara ya Ulinzi ya Taiwan imesema leo Jumatatu kuwa imenasa ndege 103 za kivita za China karibu na kisiwa hicho katika muda wa saa 24, idadi kubwa isiyo kawaida.


Kati ya Septemba 17 na 18 asubuhi, Wizara ya Ulinzi imenasa jumla ya ndege 103 za China, ikiwa ni rekodi katika kipindi cha hivi karibuni na inaleta matatizo makubwa ya usalama katika pande zote za mlango wa bahari wa Taiwan na katika kanda,” wizara imesema katika taarifa yake.


“Uchochezi wa kijeshi unaoendelea” kutoka Uchina “unaweza kusababisha kuongezeka kwa mvutano na kuzorota kwa usalama katika eneo hilo,” imeonya wizara hiyo, ambayo inaitaka Beijing “kukomesha mara moja vitendo hivi vya uharibifu vya upande mmoja.”


Kati ya idadi ya ndege za kijeshi zilizonaswa, 40 zilivuka mstari wa wastani – mpaka usio rasmi kati ya China na Taiwan ambao China haitambui – na kuingia katika zili katika eneo la utambulisho wa ulinzi wa anga wa kusini (Adiz) -magharibi na kusini mashariki, kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari. Meli tisa za kivita za China pia zilionekana karibu na kisiwa hicho

No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...