Monday, January 30, 2017

Belle 9: Baba na mama yangu ndio couple ninayoikubali zaidi

Ni couple gani ambayo unailewa zaidi hapa Bongo? Ni swali ambalo mtangazaji wa kipindi cha The Playlist cha Times FM, Lil Ommy alimuuliza Belle 9.

“Baba yangu na mama yangu,” alijibu muimbaji huyo.

“Wananivutia kwasababu nyumbani maisha ni ya kawaida lakini still baba yuko na mama halafu mara zote ambazo nimekuwa nyumbani, sijawahi kuona mama yangu anagombana na baba. Mimi nimekaa sana nyumbani kwa muda mrefu, lakini mara ya kwanza naona kama wanashikanashikana hivi ilikuwa mimi ndio chanzo, yaani mama alikuwa ananitetea mimi kwasababu baba alikuwa ananinyoosha sana sasa mama alikuwa kama anaingia hivi, lakini haukuwa ugomvi,” ameongeza.

“Kiukwezi ni best couple kwangu mimi, najifunza mengi kupitia pale, inanipa nguvu nikirudi nyumbani baba yupo, mama yupo nikitoka hapo nami nakuwa nipo fast kila kitu.”

Kwa upande wa couple ambayo haielewi ni ile ya Kanye West na Kim Kardashian.

No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...