Tuesday, January 31, 2017

Giggy Money: Mabwana wa Wema Wananishobokea Wenyewe

Kufuatia kusambaa kwa video yake akifanya vitendo vya kifuska hadharani na aliyekuwa mpenzi wa staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu, Ibrahim Mgimbu ‘Calisah’ mwanadada anayeuza nyago kwenye video za Bongo Fleva, Gift Stanford ‘Gigy Money’ amefunguka na kusema wenyewe ndiyo wanaomshobokea.

 Video hiyo chafu ya Gigy na Calisah ilisambaa hivi karibuni kwenye mitandao ya kijamii ambapo watu wengi walionekana kumshangaa mwanadada huyo huku wakimtolea maneno ya kejeli kuwa hajatulia na amekuwa akipenda kuwa kimapenzi na wanaume waliopitia kwa Wema akiwemo Idris Sultan. Baadhi ya mashabiki waliozungumza na Wikienda walifunguka kuwa, Gigy anatakiwa kubadilika kwani amekuwa mtu wa matukio kila siku na amekuwa akipita kule alikopita Wema kwa sababu alianza na Idris na sasa Calisah.

“Hivi Gigy haoni wanaume wengine hadi ajibebishe kwa wale ambao tayari walishakuwa na uhusiano na Wema? Hata sielewi Gigy anajisikiaje maana hii video yake na wanafanya vitendo vya kimahaba huku akiwa ana uhusiano na mpenzi wake wa siku zote Moj (Mourald Alpha) sijui naye huwa anaonaje na anajisikiaje anapoona mwanamke wake anafanya hivyo,” alisema shabiki mmoja aliyezungumza na Wikienda.

Baada ya kuvutiwa waya na kuulizwa kulikoni kupenda kupita alikopita Wema na kujirekodi video za kimahaba na kuziachia mitandaoni, Gigy alikuwa na haya ya kusema:
“Kwanza niseme hiyo video siku hiyo, Calisah ndiye aliyenishobokea maana ndiye aliyenifuata, kuhusu wanaume aliotoka nao Wema ni kwa sababu labda nyota yangu inamzidi maana wenyewe ndiyo wamekuwa wakinifuata kwa kifupi wanaume wa Wema ndiyo huwa wananishobokea. “Kuhusu Moj, ni mpenzi wangu na ni mume wangu mtarajiwa na ni baba wa mwanangu maana nina ujauzito wake.”

No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...