Monday, January 30, 2017

Waliookolewa mgodini watoka hospitali


Geita. Wachimbaji 15 waliokuwa wamelazwa katika hospitali ya Mkoa wa Geita kwa ajili ya matibabu baada ya kuokolewa katika mgodi wa RZ walikokuwa wamefunikwa na kifusi cha udongo kwa siku tano wameruhusiwa kutoka hospitali baada ya afya zao kuwa nzuri.

Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Brian Mawala amesema afya za wachimbaji hao zimeimarika na wana uwezo wa kuendelea na kazi.

Baada ya kuruhusiwa leo asubuhi wamekutana na Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga.

No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...