Friday, January 6, 2017

Msanii wa kwanza kusainiwa kwenye lebo ya Alikiba


Ni Abby Skillz aliyerudi rasmi kwenye muziki kwa wimbo wake Averina akiwa na Mr Blue pamoja na Alikiba amefunguka na kusema kuwa yeye ni msanii wa kwanza kusaini mkataba chini ya 'Label' ya msanii Alikiba inayofahamika kama 'Kings Music'.

  

Abby Skillz amesema hayo kupitia eNEWZ na kusema mpaka sasa label hiyo imeshasaini wasanii kama kumi ila yeye ni msanii wa kwanza kabisa kusaini chini ya uongozi wa Alikiba na kusema angeweza kuwataja wasanii wengine ambao tayari yameshadondosha wino lakini itakuwa si vyema hivyo muda utakapofika Alikiba mwenyewe ataweka wazi hilo.

"Alikiba amenitoa Kariakoo kule ni nyumbani kwa wazazi na saizi mimi niko kwake lakini nimekuja huku sababu ananisaidia mambo fulani katika muziki ambalo si jambo baya, lakini pia unapaswa kutambua mimi ni msanii wa kwanza kusaini mkataba chini ya label ya Alikiba 'Kings Music' ambayo mpaka saizi imeshasaini wasanii kama kumi hivi ila tunamsubiri Rais wetu Alikiba ndiye ataweka wazi jambo hilo" alisema Abby Skillz 


No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...