Saturday, March 11, 2017

Simulizi ya SECRET DOCUMENT(nyaraka za siri)



SECRET DOCUMENT(nyaraka za siri)
MTUNZI: BENCHRYS
SEHEMU YA PILI – 2
0758784299 wasap tu,

Tulipoishia>>>>
Baada ya Jastin kuambiwa vile na yeye hakupoteza muda akaangalia kwa njia ile ambapo lilikuja jina la JACKOB CHARLES taa za kichwa chake kilianza kupekua hili jina mara moja akagundua kwamba ni ‘bestman’ wake ambaye alikuwa ni Jakob, mara moja akanyanyua simu na kuweka sikioni ambapo kwa wakati huu sauti iliyosikika ilikuwa ni sauti ya Jakob mwenyewe ikiwa inaongea kwa furaha sana,,,,,,,,,

Songa nayo>>>
Jastin baada ya kusikia sauti ile imani yake ya kwamba yule ni rafiki yake ambae alitegemea awe ni msimamizi wa  harusi yake amempigia,
“daah sawa Bhana Jakob naona umeamua kunifanyia hivyo powa, uko wapi sasa”
“njoo kwenye ile saloon niliyokwambia”

Basi Jastin nae hakutaka kupoteza hat sekunde nyingi sana kwa mara moja akachukua gari lake prado na kuingia kisha akakanyaga moto, kisha akageuza gari lake kuelekea upande wa kutoka nje ya geti, zoezi hilo halikuwa na muda mwingi sana na kwa mara moja akawa tayari yupo nje, baada ya hapo akavaa stereo bluetooth sikioni ili imsaidie kwa mawasiliano kama kutakuwa na mtu ambae ananmpigia wakatia akiwa kwenye gari anaendesha na huo ulikuwa ni utaratibu wake na  baada ya kuvaa palepale akachukua simu yake na kuwasha bluetooth kisha akaunganisha na kile kifaa chake na kuweka simu kando, akafunga mkanda na baada ya hapo akaanza safaria mbapo ilikuwa ikimpeleka jumla kwenye saloon ambayo alikuwa ameambiwa na rafiki yake, Jakob ambaye alimweka kuwa ni msimamizi wa harusi yake ile.
‘ngrrrrrrrrrrn ngrrrrrrn’
Ni simu ya Jastin ilikuwa ikiita kwa wakati huo aliiona lakini alikuwa kwenye mwendo mkali sana na ilikuwa katika barabara kuna magari mengi sana lakini hiyo haikuwa inasababu ya kumfanya asipokee simu ile, bila kuchelewa akakwepesha jicho moja ambalo liliangalia kwenye simu na baada ya kuangalia aliweza kuona jina la  kwenye simu lililokuwa limeseviwa ‘My lover’  baada ya kuona hilo jina moyo wake ulilipukwa na furaha sana kwa kuwa ilikuwa ni simu ya mpenzi wake ambaye siku inayofuata ilikuwa ikitegemewa ifungwe ndoa takatifu. Basi hakupoteza muda akatumia mkono wake mmoja kushika usukani na mwingine akautumia katika kutafuta batani ambayo ilikuwa kwenye bluetooth ya sikion kwake ili apokee simu na hilo swla halikuwa zito sana kwake, hivo kwa sekunde tu akawa tayari ameshaigusa na baada ya hapo akaipokea simu ya Agatha,
“Darling upo wapi mbona, nipo hapa kwako sikuoni”
“nimeenda kwa Jakob mara moja, ila sio muda mwingi narudi hapo au ntakuja mwenyewe”
“hujalelewa tu kulikuwa na jambo muhimu sana la  kukwambia mpenzi ila basi, fanya uwahi kurudi basi”
“usijali mpenzi sasa hivi tu nipo hapo, alafu nadrive ntakutafuta mpenzi love u”
Jastin alifanya kuaga kwa maana mbele yake kulikuwa na traffik ambao mara zote tabia zao alikuwa akizipata sana kwa kutafutiza kosa ata kama gari lako ni salama kabisa ila njaa kwao iliwafanya wafanye mambo kama hayo,
Baada ya simu kakatwa Jastin alikuwa makini na barabara lakini aliweka nia ya kwamba anawahi kurudi kwa maana alikuwa akihitaji kujua ni jambo gani la muhimu ambalo limemfanya Agatha aondoke nyumbani kwao mpaka kuja kwake na hakujua ni kwa namn gani ameondoka mpaka afike huko kwake kwa maana haikuwa ni jambo rahisi sana kuwatoroka wazee wake kwenye mjadala mzito ambao alikuwa nao kwa muda mrefu sana, ila basi kuhus hayo hakutaka kujaji sana yeye alinyoosha mguu wake na kutaka kufika kwa rafiki yake Jakob,
Akiwa ameshawapita tena wale trafiki wa barabarani akatembea kwa hatua kadhaa simu yake ilianza kuita tena ambapo aliona ni jina la Jakob,
“huyu nae hajui kama ni po njiani” alijisemea Jastin na baada ya hapo ya hapo kapokea simu na kutomwachia nafasi ya kuongea yule ambea alikuwa akimpigia kwa wakati ule,
Ni baada ya kubinyeza tu batani ile ya bluetooth yake,
“Jakob niko njiani sasa hivi nafika”
Aliongea na kubonyeza tena ambapo simu ilikatika bila kusikia sauti ya upande wa pili, yeye safari yake alihitaji ikamilike ili akaongee mengi sana na Jakob na sio kwanjia ya simu na hiyo  ndio ambayo ilimpelekea yeye kukata simu yake kwa mara moja bila kumsikiliza Jakob, mwendo wake kwa kuwa ulikuwa ni mkali sana akawa tayari amefika kwenye saloon ambayo ilikuwa  ameambiwa na Jakob na baada ya kufika pale akafika na kutoa simu yake ili apige, lakini kabla ya yeyey kupiga simu yake ikaanza kuita tena, na alipo tazama jina lilkuwa limeseviwa jako2, akili yake ilishapembua akajua yule ni Jakon kwa namba yake mpya baada ya kuona vile kapokea na kuweka simu sikioni ambapo alisikia sauti toka upande wa pili ikisema “ingia tu nipo ndani” mpaka hapo Jastin hakuw ana nafasi yakuuliza mara ya pili kwa maana alishakuwa amepewa ruhusa na kwa maana alikuw ani tayari amemwona hivyo yeye akanyoosha jumla mpaka ndani ambapo alimwona Jakob akiwa amekaa kwenye sehemu maalumu ya kurekebishia nywele ili zikae katika  mwonekano ambao ni mzuri sana kwa kijana au mzee yeyote kulikuwa na dada mmoja ambae alikuwa nyuma yake anamseti nywele huku akiwa anamfanyia scrab safi kabisa, Jakob kwa jinsi alivyokuwa ametulia usingeweza kudhani kama anaondoka na alikuwa kama ametua shida zake zote, lakini baada ya kuhisi kuna mtu ameingia ilimpasa kushituka kidogo kwa maana alijua ni tayari Jastin ameshaingia pale ndani,
“ooh wao Jastin karibuuuu ila umekawia hatari yani”
“aaa wai sijakawia wala nini sema tu haraka zako na hata umenistukiza”
“daaah habari za huko lakini, ivi ninasiku ngapi sijui sijawatembelea”
“daah tatu ila hujanisusa sana ndugu, dada habari yako” aliongea Jastin na kutupa salamu kwa mtu aliyekuwa akimhudumia Jakob kwa wakati ule
“salama tu kakaangu, karibu ukae chini”
“ooh wao asante”
“vipi shem hawa ndio wenye tukio kesho eeh” ilikuwa ni sauti ya yule mhudumu wa huduma ya kuset nywele na mambo mengine ambapo alikuwa akiuliza kwa Jakob,
“yaah ndio shem wetu huyo kesho anafunga pingu za maisha, vipi mbona umeliza hivyo”
“mmh jamani kuuliza kosa kwani?”
“powa basi ushajua ila na wewe mwongo kwani hukuona ata picha zao?”
“aah acha sikujua mimi< shem heshima yako mahala pako  ni hapa usikae tena huko maana wewe inatakiw aupendeze zaidi yani, wifi mzima?”
Aliongea yule dada huku akiwa anageukia kwa Jastin na kumwonesha kiti ambacho kilikuwa ni maalumu kwaajili ya kupunguza na kuset aina nzuri ya mnyoo utakao kuwapowa sana kwa mtu kama Jastin,
Jastin nae hakuwa na kipingamizi akasimama na kukisogelea kiti kile na baada ya hapo akakaa ili nae aanze kufanyiwa kazi nzuri,

Wakati huo Agatha alikuwa nyumbani kwake akiwa badoa  namngoja Jastin lakini baada ya kukaa sana akagundua huyu hawezi kuwahi hata mara moja, mara moja akachukua kibegi chake kidogo ambapo safari yake ilikuwa kuekelea nyumbani, lakin baada ya kufika kwenye eneo jilani na alipoliacha gari lake,akaonahali ya tofauti ambapo kuna magari mengine mawili yalikuwa yamepaki na hakujua ni akina nani ila akajitoa wasiwasi kwa kuchukulia maana ya kwamba nao watakuwa wanamishe zao mitaa ile,
Agatha alikuwa akiendelea kusogea kwa taratibu mpaka kufikia lile gari ambapo alianza kutoa funguo yake kwenye pocho yake ili akifika pale awe na kazi moja ya kuchokonoa tu gari lake  ili aondoke nalo ili awahi nyumbani,
Hatua moja baada ya nyingine alianza kutembea na kuikaribia gari lake, muda mfupi akawa tayari amefika alitoa funguo zake na baada ya hapo akasogelea mlango huku akishika kitasa cha gari, lakini akajikuta akipigwa na kitu kizito na hapohapo alipoteza fahamu palepale.
               *****

“ndio hivo yani inatakiwa uwe kawaida tu tena hiyo kesho  kujiamini ndio mpango mzima, kuna jamaa aliwahi kunambia eti anakunywa ili awe anawaona watu wote ni kama wadogo zake”
“hahahaaa mi na pombe ni maadui wakubwa sana asee na sihitaji kabisa kwa maana naona ni kama haina faida kwangu, we fikiria ninamawazo ya kuwa na shida ya pesa halafu naenda bar ili tu ninywe eti kupoteza mawazo hiyo hela ningetunzwa siingeongezea baadhi ya kiasi ambacho nilikuwa nakihitaji”
“daaah unamawazo fulani Jastin hadi nimeielewa point yako, zamani mi nilikuwa naona tu baba akinywa na kusema eti pombe ni tamu sana ila kuna siku moja nikataka kuthibitisha kwa kuonjwa duuh mbona nilitema mate mi mwenyewe ata kama haikuwa na harufu mbaya, kwa maana nikali hatari ila wao sijui wanapenda ya nini”
“ hiyo kesho  naingia kama nilivyo wala siwezi kunywa watu ni wakawaida wote hawa tena nafahamu kabisa”
“yaah hivyo ndio inatakiwa pombe inaweza sababisha kuvunja heshima kwa umati wawatu na kusababisha mambo mengine”
“ni kweli kabisa yani”
Yalikuwa ni mazungumzo kati ya Jastin na Jakob kule saloon, na Jastin kuhusu habari ya Agatha hakuwa akijua chochote, yeye alikuwa tu na amani zote kwanza aliamini kama Agatha akikaa na kuona yeye anachelewa basi ata simu atampigia kwahiyo hakuna shida yoyote ile, alijifariji na baada ya hapo mambo mengine yaliendelea, huku yule dada akiwa kimya tu kuwatengeneza vizuri kadiri ya kazi yake ilivyokuwa ikimpasa kuifanya kwa mana alikuwa akifahamika sana na alikuwa na jina kubwa sana kwa Njombe na baadhi ya maeneo mengine ambako alikuwa amewahi kupewa nafasi yakumfanyia mtu urembo kwaajili ya maandilizi ya harusi au tafrija yeyote ile na licha kuwa na saloon kubwa hiyo badio alikuwana wanafunzi wake ambao wao walikuwa wakihusika na kupamba kwenye maharusi na kuandaa mahali husika ili pawe ni pakuvutia kushawishi waalikwa wa sherehe yenyewe,
Jastin bado alikuwa ametulia huku stori za hapa na pale zikiwa zinaendelea, na baada ya muda ambao ulikuwa si wa kuwachosha sana kazi ilikuwa tayari imeshaisha kabisa, Jastina alisimama na kujiweka sawa lakini akiwa anafanya vile mara simu yake ikaita alipotazama mpigaji alikuwa ni Ngosha,
“hallow Ngosha”
“uko wapi wewe, shem amekuja hadi ameondoka tayari”
“daah ameshaondoka” aliuliza swali la pili huku akijua kabisa nini ambacho kiliongelewa na kweli alikuwa amechelewa sana,
“ndio ameondoka na Dogo amepiga simu kwamba hatawezakuja ila atatuma zawadi”
“daaaaah tayari Yona ameshaniangusha tayari ila sio mbaya nitampigia simu”
Ngosha na Jastin hawakuongea sana simu ya Jastin ilianza kuita ambapo mpigaji alikuwa ni mama yake mzazi, Jastin aliipokea na kuweka sikioni lakin cha ajabu hakusikia sauti yoyote ikiongea, lakini baada ya muda kidogo akasikia sauti ya kike ikiwa inalia,
“mama, mama, mamaaaaa halow kuna nini”
Jastin alipiga ukunga lakini hakuitikiwa na yeyote,,,,,,,,,,
…………itaendeleaa


No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...