Thursday, March 9, 2017

Simulizi ya SECRET DOCUMENT(Nyaraka za siri)


SECRET DOCUMENT(Nyaraka za siri)
MTUNZI: BENCHRYS
SEHEMU YA KWANZA – 01
0758784299 wasap tu,
,,,,,,trailer,,,,,
Katika kanisa moja kulikuwa na marumbano baina ya wachungaji waliokuwa watatu na katika marumbano yao yalipelekea mpaka kushikana na kila mmoja hakutaka kukubali kama mwenzake anaweza kumzidi,
“nimesema usinizoee kama lile dili tulisha limaliza sasa tatizo lako nini?”
“ahaaa sasa ngoja nikuonyeshe boya wewe”
“nani boya, nani boya nakuuliza mpuuzi kweli ivi kwakuwa unawaamini wengi unadhani ndio itakuwa ni njia rahisi sana kwako wewe kunishinda mimi, nielewe mbogo wewe mimi ni zaidi yako tena ngoja”
Baada ya kuongea alisimama na kama nyani na kuruka mateke ambayo yalikuwa dabo na kumtulizia mchungaji mwenzake kwenye kifua na hiyo ilikuwa ni kama amemvizia penyewe kwa maana yule mwenzake palepale aliaguka chini huku akiwa anatoa povu jeupe mdomoni kwake,
Baada ya mwenzake kuona amefanya kitendo kama kile hakutaka kupoteza muda hata kwa sekunde moja, palepale akaondoka na kwenda kwenye stoo ya kuhifadhia nguo za kichungaji kabla ya kuvaa na baada ya hapo akaangalia tambala fulani lilikuwa jeupe na kuja nalo kisha akamvalisha yule mchungaji ambaye alikuwa akitoa povu mdomoni kisha akamchukua na kwenda kumwingiza kwenye sanduku fulani ambalo lilikuwa ni la kioo kizito sana,
----secret document----
Ni katika mkoa mpya wa Njombe wilaya ya Njombe Mji, kata ndogo ya Mjimwema kulikuwa na familia ya watoto wa wanne ambapo kila mtoto alikuwa na kazi yake baada ya kuwa wamesoma na kufanikiwa kwa kiwango ambayo kilikuwa kimewaridhisha wao, familia ilikuwa na watoto wanne ambapo majina yao yalikuwa ni Agatha, Dorice, Yona na mmoja ambaye alikuwa wa mwisho ni happy.
Watoto hao wote walikuwa na hali nzuri sana kiafya kimaisha pamoja na mambo mengine, kila siku kulikuwa na maelewani mazuri sana baina yao hao wanne ambapo familia ilikuwa na wasichana watatu huku kukiwa na mvulana mmoja kama kaka yao kwa heshima tunaita hivo.
Maisha yao yalizidi kusonga huku kila mmoja akiwa anafurahia sana kuishi kwa amani na mwenzake, ambapo mwaka 2009 dada yao ambaye alikuwa ni mkubwa wa wote katika familia alitangaza kuwa anatarajia kumtangaza mmewe mpendwa ambaye alikuwa anampenda kwa moyo wote, haikuwana mfano wa kufananisha na mwanaume yeyote kwa jinsi alivyokuwa akimpa asilimia nyingi sana katika moyo wake, mmewe alikuwa akifahamika kwa Jina la Jastin, ambaye nae alikuwa ni wa kutoka dar,
Matangazo yalitangazwa kila mahali hususani kanisani na mahali pengine marafiki zake wengi sana walialikwa kushiriki kwenye ndoa hiyo takatifu, tarehe zilisogea kwa haraka sana ambapo harusi hiyo ilikuwa ni ya tarehe 20/06/2009 siku ya jumamosi,
Katika kuendelea na utaratibu wa kuandaa ndugu na maandalizi baadhi kila mtu alikuwa na makini sana na jukumu ambalo alikuwa amepangiwa na wakubwa,
Agatha yeye alikuwa na jukumu la kuwapigia ndugu na marafiki zake na baadhi ya maclassmate ambao alikuwa akiwakumbuka kwamba walisoma wote, pindi yupo shuleni,
Siku hiyo ilikuwa ni ijumaa kuikaribisha jumamosi ambapo jumamosi ndio ilikuwa ni siku maalumu ya tukio lenyewe, baadhi ya marafiki na ndugu wa jilani walikuwa tayari kwenye nyumba ya akina Agatha,
Dorice yeye alikuwa na kazi ya kwenda kununua kila kitu ambacho kitakuwa kimesalia na ndio ambaye alijua kila ratiba, safari zake nyingi ilikuwa ni kwenda sokoni na kurudi huku akiwa na simu yake sikioni huku anawapa taarifa baadhi ya mrafiki zake.
Nyumba ya jastin na Agatha ilikuwa nii ndogo sana kutokana na kutokana na wageni ambao walikuwa wamefurika lile eneo kutoka pande nyingi sana ikiwemo marafiki wa Jastin upande wa kiume pamoja na wazazi na ndugu baadhi, walikuwa na furaha sana bado Agatha alikuwa anajifikiria hii siku ya kesho itakuaje. Kwamaana hakuwahi kuolewa au kujumuika kwa ujilani sana kwenye shughuli kama hizo. Muda wote yeye alikuwa akingoja tu wamama ambao walikuwa nje ndio wawe waendeshaji wa kila kitu na kubwa ambacho kilikuwa kikifanya mambo yote kuwa sawa kabisa ni kamati kadhaa ambazo walikuwa wameziweka kwa ajili ya muziki, chalula, mapambo na kadhalika,
Yote ilifanywa kwa kutumia gharama kubwa sana na kuhakikisha mambo yanaenda sawa sawia,
“ok ok powa shogaangu usikawie hiyo jamani siunajua tena, alafu kna simu inaingia naomba ukate basi niipokee”
Alikuwa ni Agatha akiwa anaongea kwenye simu yake na hapo akapokea simu nyingine ambapo nayo haikuchukua muda sana,
Jastin nae muda wote alikuwa hayupo mbali sana, alikuwa amekaa na marafiki zake kadhaa ambapo kulikuwa na ngosha wa mtaa uleule wa mjimwema, jina hili alipewa kwa kutokana na kuwa na uwezo mkubwa sana wa kuimba/ kuchana mistari mingi sana ya msanii wa hip hop hapa Tanzania anafamika kwa jina la Fid Q, na jina lake la A.K.A lilikuwa ni NGOSHA hivo nae alipewa jina hilo na kila mtaa alikuwa akifahamika kwa jina hilo,
“asee hivi Jakob umemwona wapi maana nangoja simu yake na wala hapigi,a sije niyeyusha na kesho hiyo maana daah ninahamu sana na siku hiyo”
Aliongea Jastin ambapo alikuwa n kama akimuuliza ngosha na wenzake,
“we usijali tena ngoja nimpigie kabisa kwa maana huyu mkuu nae kwa kuvuta masaa hajambo kabisa,
“daah kweli fanya hivo”
Aliongea Jastin na kunyanyua simu yake ambapo ilikuwa inaita kwa wakati ule kwa namba ngeni,
“mmh nani nae huyu anataka kuleta gezi hapa”
Aliongea Jastin na baadae akageuza simu kuelekea kwa Ngosha, “oya hii namba unaipata?”
“apana ndugu yangu mpokee sikiliza anaongea nini” ulikuwa ni ushauri kutoka kwa Ngosha kwa wakati ule ambapo na yeye alikuwa akihangaika kutafuta namba ya Jakob ili apige na kujua mahali alipo kwa maana alikuwa ameombwa kuwa kama msimamizi au ‘bestman’ kwa siku hizi lilivyozoeleka hili neno,
Jastin hakutaka kupoteza muda sana akapokea simu na kuiweka sikioni ambapo alitulia kimya na kuanza kusikiliza kwa umakini sana ili kujua ni nani anae piga simu kwa wakati ule,
“tafadhali Jastin mbona huongei”
Ilitoka sauti kwenye upande wa pili wa simu ambapo hayo yote yalikuwa yakisikika kwa Jastin lakini alijalibu kuvuta kumbukumbu huyo ni nani anaeongea lakini hakujua bado kwa maana sauti ilikuwa ni ngeni sana kwake, Jastin bado hakutaka kujibu ikiwa hafahamu kabisa mpigaji wa simu ni nani kwa wakati ule,
“hallo Jastin au nakosea namba!!!”
Bado sauti ya upande wa pili haikukata tamaa kwa kuendelea kuongea na Jastin ili iitikiwe,
Jastin baada ya kuona anakaziwa vile akaamua kuongea na,
“Tafadhali ndugu namba ngeni kwani nani mwenzangu?’
“hahahaaaah kumbe sijakosea. Saaasa nilikuwa na ombi kwako Jastin rafiki yangu najua utakuwa umenisahau lakini hakuna tatizo utanikumbuka endapo tutaonana,” akatulia na kuvuta pumzi kidogo kisha akaendelea, “usije sema naongea mengi sana, kaka Jasi eeh kwasasa upo wapi?”
Swali hili lilifanya Jastin ashitule kidogo kwa maana yeye katika kumbukumbu zake alikuwa akikumbuka sauti ya kila rafiki yake na kama kwa ile ingekuwa ni ngeni basi ilipasa aanze kwa kujitambulisha kwanza kwa maana huondio ulikuwa ni utaratibu wake katika simu zozote ambazo alishazoeana na marafiki zake, kiufupi alibaki katika sinto fahamu hakujua bado afanye nini ili kukumbuka huyu ni nani, na kwa gafla tu alijawa na upole kwa maana alijitahdi kukumbuka lakini bado ikawa ni shida kwa upande wake,
“Jastin unawaza nini wakati siku imebakia moja tu, punguza mawazo nduhu yangu hebu jipe shavu kama mimi Ngosha nikiwa namtukuza babu langu ze doni”
Maneni ya Ngosha yalikuwa ni kama ya kufurahisha lakini ndani yake yalikuwa ni ukweli mtupu kwa maana ni kweli hua anamsifu sana Fid q kwa mistari yake kila awapo kwenye kundi la masela wenzake ambao wanapenda sana mziki wa namna hiyo na baadhi ya maeneo ambayo yanaweza yakawa na battle au mashindao juu ya kuchana,
“usishangae sana Ngosha ile namba ni kama siielewi vile kwa maana nimepokea lakini sijamwelewa na sijui ni nani ila yeye anadai kunifahamu vyema sijui nani huyu”
“hhhaaaaha Jasi eeeh acha hizo namba ya mtandao gani hiyo?”
“hii ni sifuri saba hamsini na nne(0754___) nadhani ni voda hii au siyo”
“basi kazi kwisha angalia kwa kifanya kama unatuma pesa kwa hiyo kwenye M-PESA lakini kwenye salio andika salio ambalo linazidi kwenye kiwango ambacho unacho m-pesa huko kisha itume kwa kuthibisha namba moja, kazi simpo tu wataleta jina lake na utajua tu”
“aah kumbe rahisi namna hiyo, ngoja kwanza”
Baada ya Jastin kuambiwa vile na yeye hakupoteza muda akaangalia kwa njia ile ambapo lilikuja jina la JACKOB CHARLES taa za kichwa chake kilianza kupekua hili jina mara moja akagundua kwamba ni ‘bestman’ wake ambaye alikuwa ni Jakob, mara moja akanyanyua simu na kuweka sikioni ambapo kwa wakati huu sauti iliyosikika ilikuwa ni sauti ya Jakob mwenyewe ikiwa inaongea kwa furaha sana,,,,,,,,,
………..itaendelea
Ni mwanzo wa stori ya ‘’’’’’’secret document’’’’’’’’’’


No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...