Wednesday, March 1, 2017

Rasmi sasa Mama Diamond Atua Bongo Muvi,Hii Ndio Muvi Yake ya Kwanza atakayo cheza.




Mama mzazi wa staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’, ametua rasmi kwenye fani ya uigizaji wa sinema za Kibongo (Bongo Muvi).

Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalum, mama Diamond alitamba kwenda kimataifa kwenye upande wa filamu kama anavyofanya mwanaye Diamond akiwa ameshiriki katika utayarishaji na uigizaji wa filamu iitwayo Mtepela iliyochezewa huko Kibirizi mkoani Kigoma.

“Nimefanya hiyo filamu na wasanii wa Kigoma, nawajua vizuri lakini kwa sasa siwezi kuizungumzia zaidi,” alisema mama Diamond.

Kwa upande wa mtayarishaji aliyeshirikiana naye aliyejitambulisha kwa jina la Isaya Lazaro almaarufu Zito, alisema mama Diamond mbali na kushiriki katika utayarishaji wa filamu hiyo pia alitoa fedha na ni mmoja wa waigizaji waliofanya vizuri ndani yake.

“Tulimwandalia scene (vipande), akavicheza lakini kabla ya kumaliza alipata safari ya kwenda Afrika Kusini na baada ya kurejea tuendelea kuimalizia”, alisema Zito.


No comments:

Post a Comment

New Posts

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

  Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbw...