Saturday, September 21, 2024

IJUE SCANIA P380[Mende]




Scania P380 Mende ni nini?

Scania P380 ni mojawapo ya malori maarufu yaliyoundwa kwa nguvu na ufanisi wa hali ya juu, hasa kwa mazingira ya kazi ngumu kama vile usafirishaji wa mizigo mizito. Aina ya Scania P380 Mende imepewa jina kutokana na muonekano wake wa kipekee wenye nguvu, na uwezo wa kufanya kazi kwenye mazingira magumu, ikiwa ni pamoja na barabara mbovu na maeneo ya milimani.

Sifa Kuu za Scania P380 Mende

  1. Injini: Scania P380 ina injini yenye uwezo wa kutoa nguvu kubwa inayofikia 380 hp, inayowezesha kubeba mizigo mizito bila kupunguza ufanisi wa mafuta.
  2. Ubebaji Mzigo: Lori hili lina uwezo wa kubeba mizigo mikubwa na hutumiwa mara nyingi katika usafirishaji wa mchanga, mawe, na bidhaa nyingine nzito.
  3. Muundo wa Chassis: Chassis yake imara inafaa kwa kazi katika mazingira magumu kama ya ujenzi, migodi, na kilimo.
  4. Mfumo wa Kinga ya Uvutaji wa Mafuta (Fuel Efficiency): P380 imeundwa kuhakikisha kuwa ina matumizi bora ya mafuta licha ya ukubwa na nguvu yake.


Matumizi ya Scania P380 Mende Tanzania

Katika mazingira ya Tanzania, Scania P380 Mende ni maarufu sana kwa shughuli zifuatazo:

  1. Usafirishaji wa Vifaa vya Ujenzi: Kutokana na miradi mingi ya ujenzi inayoendelea nchini Tanzania, lori hili linatumika sana kusafirisha mchanga, kokoto, saruji, na vifaa vingine vizito.
  2. Migodi: Katika migodi ya Tanzania, Scania P380 ni chaguo maarufu kwa ajili ya kusafirisha mawe, makaa ya mawe, na madini mengine. Uwezo wake wa kuhimili uzito na mazingira magumu hufanya kuwa bora kwa kazi hizi.
  3. Kilimo: Wakulima wakubwa hutumia Scania P380 kusafirisha mazao kama vile mahindi, mpunga, na bidhaa nyingine za kilimo.
  4. Usafiri wa Mizigo Mizito: P380 hutumika sana kusafirisha mizigo mizito ya kibiashara kati ya miji mikubwa na bandari, hasa katika Dar es Salaam, Arusha, na Mwanza.


Gharama za Ununuzi na Unafuu wake kwa Watumiaji

Gharama ya Scania P380 Mende hutofautiana kulingana na umri, hali ya gari, na iwapo limeagizwa jipya au limetumika. Bei ya Scania P380 jipya inaweza kufikia TZS 200 milioni hadi 300 milioni, kutegemea vipengele vilivyoongezwa na huduma maalum.

Kwa magari yaliyotumika, bei inaweza kuanzia TZS 80 milioni hadi 150 milioni, kutegemea na hali ya gari, miaka ya matumizi, na matengenezo yaliyofanyika.

Unafuu kwa Watumiaji

  1. Matumizi ya Mafuta: Ingawa Scania P380 Mende ina injini yenye nguvu, inajulikana kwa ufanisi mzuri wa matumizi ya mafuta. Hii inamaanisha kwamba gharama za uendeshaji kwa muda mrefu ni nafuu ukilinganisha na malori mengine ya ukubwa sawa.
  2. Matengenezo: Sehemu za magari ya Scania zinapatikana kwa wingi nchini Tanzania, na kuna mtandao mkubwa wa mafundi waliobobea katika magari haya. Pia, Scania imeunda magari yake kwa njia ya kuhitaji matengenezo ya mara chache, jambo linalopunguza gharama za matengenezo kwa muda mrefu.
  3. Uwezo wa Kubeba Mizigo Mikubwa: Uwezo wa kubeba mizigo mikubwa kwa ufanisi na haraka hupunguza idadi ya safari zinazohitajika, hivyo kuokoa muda na gharama za mafuta.
  4. Thamani ya Uwekezaji: Ingawa gharama ya ununuzi wa awali inaweza kuwa kubwa, P380 ni gari ambalo hudumu kwa muda mrefu na huendelea kuwa na thamani nzuri hata baada ya miaka kadhaa ya matumizi.


Hitimisho

Scania P380 Mende ni moja ya magari bora kwa matumizi ya biashara nchini Tanzania, hasa kwa sekta ya ujenzi, madini, na kilimo. Gharama ya ununuzi wa awali inaweza kuonekana kuwa kubwa, lakini unafuu wake kwa watumiaji unatokana na ufanisi wa mafuta, matengenezo ya mara chache, na uwezo wa kubeba mizigo mikubwa. Kwa wamiliki wa biashara zinazohitaji usafirishaji wa mizigo mizito, gari hili ni uwekezaji mzuri kwa muda mrefu.

Monday, September 16, 2024

Unaijua safaru?

 



Sasa Mwaka 1696 - 1701, Sir Isaac Newton aliajiriwa katika kampuni maalumu 'Royal Mint' nchini Uingereza inayozalisha sarafu.


Kwa kipindi hicho inaelezwa nchini Uingereza kulikua na tatizo kubwa la uwepo wa sarafu bandia na hivyo kufanya uchumi wa nchi kudorora. Newton aliajiriwa kwaajili ya kuleta suluhisho la tatizo hilo.

Alichofanya ni kuanzisha utaratibu wa kuweka matuta pembezoni mwa sarafu, lakini inaelezwa hapo nyuma sarafu zilikua zinawekwa matuta ila sio kwa mfumo ambao Newton aliamua kuutumia.

Faida za matuta hayo;

- Ni rahisi kugundua sarafu bandia kwa kile kinachoelezwa kuwa ni ngumu ku sampo' matuta kufanana sawa na sarafu halisi. Hata uki sampo' lazima kutakua na utofauti wa uzito na muonekano!

- Matuta hayo pia yanasaidia sarafu kuwa ngumu kujikunja kirahisi na hivyo kufanya kudumu kwa muda mrefu zaidi kwenye mzunguko.

- Pi matuta hayo huwasaidia watu wenye ulemavu wa macho ili kuweza kugundua kwa urahisi aina mbalimbali ya sarafu.

Fahamu kuhusu Homa ya Kuchekacheka.

 



Ugonjwa wa kuchekacheka ulitokea kwa mara ya kwanza mwaka 1962 katika shule ya Kashasha, wilayani Muleba, Tanganyika. Wanafunzi wa kike walikuwa wanacheka ovyo bila kujizuia.


Shule ilifungwa, wanafunzi waliporudi makwao waliwaambukiza ndugu na majirani, tatizo hilo liliendelea kwa karibia mwaka mzima. Lilikuja kutokea tena mwaka 2007 katika shule mbali mbali.


Inaelezwa kuwa msongo wa mawazo ilikuwa ni sababu kuu ya tatizo hilo.

Source: #Fahamuzaidi #Fahamumedia


Pombe, Siraga sio visababishi vikuu vya saratani

 



DAKTARI Prudence Kiwia kutoka Taasisi ya Saratani Ocean Road (ORCI) amesema pombe na sigara si vyanzo vya saratani; wengi wanaougua hawakuwahi kutumia vilevi hivyo.



Amesema saratani zinazoongoza kila mwaka ni za shingo ya kizazi na matiti kwa wanawake na tezi dume kwa wanaume, hivyo jamii inatakiwa iwe na tabia ya kufanya uchunguzi kila wakati. 


Dk. Kiwia alisema hayo jana jijini Dar es Salaam baada ya kupokea msaada wa vifaa mbalimbali na mashine kutoka Taasisi ya Jema Foundation iliyotembelea taasisi hiyo kwa ajili ya kuwafariji wagonjwa. 


"Tumefurahi sana tumepokea misaada mingi kwa wagonjwa wetu, lakini kubwa ningependa kusisitiza wananchi kwa ujumla kwa sababu saratani ni hatari sana na njia bora ya kujikinga na saratani ni kufanya uchunguzi.


 "Visababishi vingi vya saratani havionekani, wengi wanaongelea pombe na sigara, lakini si anayevuta sigara na kunywa pombe ndiye anaishia kupata saratani, hapana! Tuna wagonjwa wengi wanapata saratani, hawajawahi kutumia (sigara au pombe) alisema Dk. Kiwia.



 Aliwataka wananchi kufanya uchunguzi mapema wanapoona mabadiliko yoyote kama vile uvimbe au kupata uchafu sehemu za siri. 


"Kwa mwaka tunapata wagonjwa wengi sana, hasa shingo ya kizazi, maziwa kwa wanawake na kwa wanaume tezi dume, hao ni wengi sana, siwezi kukupa hata mfano kulinganisha na saratani zingine kama mfumo wa chakula, kichwa... ni wachache sana," alisema.  


Awali Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Jema Foundation, Jema Baruan, alisema alikuwa mgonjwa wa saratani na alipona miaka minane iliyopita, na kwamba aligundulika kuwa na maradhi ya saratani ya mitoki inayoadhimishwa kila mwaka Septemba 15. 


Alisema wameamua kuwatembelea wagonjwa wenye saratani ili kuwapa faraja na matumaini na pia wamewapelekea baadhi ya mahitaji yakiwamo magongo, viti vya wagonjwa, mashine ya sukari, mashine ya kupima mapigo ya moyo (BP) na vitu vingine. 



"Nimepitia hivi, ninamshukuru Mungu nimeweza kuikabili saratani ya mitoki na nimepona, lakini yupo mwingine ambaye anapambana na ni Mtanzania kama mimi, nikaona si haba na yeye tuje tumguse kwa sababu matendo ya huruma ndiyo matendo yanayompendekeza Mungu.


"Asilimia kubwa hawaponi lakini kuna asilimia ndogo iliyobakia wanapona, mimi nilifanya tiba ya chemotherapy ambayo ilikuwa na mizunguko 16, sikuacha tiba katikati, nilikuwa nakula ipasavyo unakuta mtu anafanya tiba, lakini hali chakula ipasavyo, tiba inamzidia," alisema Baruan.  


Alisema mgonjwa anatakiwa ale vizuri na kufanya mazoezi pamoja na kusikiliza ushauri wa daktari, akionya kuchanganya huduma za hospitalini tiba za kienyeji. 


"Mimi nilijikita kwenye tiba niliyoambiwa, nikafanya mazoezi, nikala vizuri nilikuwa ninajilazimisha kula, changamoto ilikuwa kwenye kula, mgonjwa unatakiwa ujilazimishe kula, bahati nzuri nimepona," alisema. 



 Mwakilishi wa Kampuni ya Big Bon, Ahmed Salum alisema wagonjwa wa saratani wanateseka, hivyo wameona kuwachangia chochote kwa kuwaonesha upendo.

Monday, September 18, 2023

Libya yatangaza hali ya dharura ya mwaka mzima baada ya mafuriko

 


Serikali ya Libya imetangaza hali ya dharura ya mwaka mzima kwa shabaha ya kuzuia kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokuumbwa na mafuriko makubwa ya mashariki mwa nchi hiyo.


Jumapili iliyopita, kimbunga cha “Daniel” kilipiga maeneo kadhaa mashariki mwa Libya, na hasa hasa miji ya Benghazi, Al-Bayda, Marj, Susa, Shahatt na Derna.


Baada ya kimbunga hicho, Shirika la Afya Duniani lilionya kuhusu kuenea magonjwa ya kuambukiza katika maeneo yaliyokumbwa na kimbunga na mafuriko hayo.


Kwa mujibu wa shirika la habari la IRIB, Haidar al-Sayeh, mkuu wa Kituo cha Taifa cha Kudhibiti Magonjwa nchini Libya, alitoa taarifa na kutangaza idadi ya sumu ambazo zimeripotiwa kutokana na matumizi ya maji ya kunywa huko Derna, Libya.


Akizungumzia kutotumika maji ya kunywa katika jiji la Derna, Al-Sayeh amesema kuwa, hali ya hatari ya mwaka mmoja itatangazwa katika maeneo yaliyoathiriwa na dhoruba na mafuriko mashariki mwa Libya ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa wowote wa kuambukiza katika maeneo haya.


Shirika la Afya Duniani lilitangaza siku ya Jumamosi kuwa, zaidi ya watu 9,000 wametoweka katika mji wa Derna mashariki mwa Libya.


Idadi ya waliofariki kutokana na kimbunga hicho nchini Libya hadi sasa imetangazwa kuwa zaidi ya 11,000.

Taiwan yanasa ndege 103 za kivita za China kwenye anga yake



 Wizara ya Ulinzi ya Taiwan imesema leo Jumatatu kuwa imenasa ndege 103 za kivita za China karibu na kisiwa hicho katika muda wa saa 24, idadi kubwa isiyo kawaida.


Kati ya Septemba 17 na 18 asubuhi, Wizara ya Ulinzi imenasa jumla ya ndege 103 za China, ikiwa ni rekodi katika kipindi cha hivi karibuni na inaleta matatizo makubwa ya usalama katika pande zote za mlango wa bahari wa Taiwan na katika kanda,” wizara imesema katika taarifa yake.


“Uchochezi wa kijeshi unaoendelea” kutoka Uchina “unaweza kusababisha kuongezeka kwa mvutano na kuzorota kwa usalama katika eneo hilo,” imeonya wizara hiyo, ambayo inaitaka Beijing “kukomesha mara moja vitendo hivi vya uharibifu vya upande mmoja.”


Kati ya idadi ya ndege za kijeshi zilizonaswa, 40 zilivuka mstari wa wastani – mpaka usio rasmi kati ya China na Taiwan ambao China haitambui – na kuingia katika zili katika eneo la utambulisho wa ulinzi wa anga wa kusini (Adiz) -magharibi na kusini mashariki, kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari. Meli tisa za kivita za China pia zilionekana karibu na kisiwa hicho

Askari wa kike Tanzania washiriki mkutano wa mwaka 2023 New Zealand

 Askari wa kike kutoka nchini Tanzania wameshiriki mkutano wa mwaka 2023 wa mtandao wa polisi wanawake duniani (IAWP) nchini New Zealand.



Mkutano huo umebeba kaulimbiu isemayo” Refresh, Renew,Refocus umefunguliwa September 17,2023 mji wa Auckland.





Aidha Mkutano huo umeudhuriwa na mataifa 65 yakiwemo mataifa mengine kutoka Afrika kama vile Tanzania,Ghana na Africa Kusini.





Itakumbukwa mwishoni mwa mwezi Julai Tanzania ilikuwa mwenyeji wa mkutano kama huo kwa ukanda ya Afrika uliyofanyika jijini Dar es salaam na kuleta matokeo makubwa ya kiutendaji kwa maafisa na askari wa kike ambao walishiriki na mada mbalimbali kufundishwa lengo likiwa kuwaongezea uwezo na maarifa ya kiutendaji.





Mkutano huo uliofunguliwa leo septemba 17,2023 katika mji Auckland Nchini New zealand unaoambatana na mafunzo ya kuwajengea uwezo askari wa kike, sambamba na kutoa fursa na kutengeneza mtandao wa mawasiliano kwa wasimamizi wa sheria.





Mbali na hilo Ujumbe huo kutoka Tanzania uliongozwa na Kamishna wa Polisi CP Suzan Kaganda wa kamisheni ya Utawala na rasilimali watu umetumia mkutano huo kutangaza utalii na vivutio vya kitamaduni vilivyopo Tanzania.



Mkutano huo hutahitimishwa Septemba 21,Mwaka huu.



Urusi yazuia mashambulizi mapya ya ndege zisizo na rubani za Ukraine

 


Urusi imedai kuangusha ndege kadhaa zisizo na rubani za Ukraine katika eneo lililokaliwa la Crimea, katika mkoa wa Moscow pamoja na ile ya Belgorod na Voronezh, karibu na Ukraine.


Ndege kadhaa ziliharibiwa katika eneo lililounganishwa la Crimea, katika mkoa wa Moscow na ile ya Belgorod na Voronezh, usiku wa Jumapili kuamkia leo Jumatatu.


“Drones zilinaswa juu ya maeneo ya magharibi, kusini-magharibi, kaskazini-magharibi na mashariki mwa peninsula ya Crimea, Istra (magharibi) na Domodedovo (kusini) wilaya za mkoa wa Moscow, mikoa ya Belgorod na Voronezh (kusini-magharibi),” Wizara ya Ulinzi ya Urusi imesema kwenye Telegramu, bila kubainisha idadi ya ndege zilizoharibiwa au kuripoti uharibifu au majeruhi kufikia hatua hii.


“Vituo vya uzalishaji wa kiwanda cha kivita cha Kharkiv, ambapo ukarabati na utunzaji wa magari ya kivita ya Kikosi cha Wanajeshi wa Ukraine ulikuw ukifanyika, vlipigwa na mashambulizi haya anga,” chanzo hicho pia kimetangaza.


Hapo awali, mkuu wa utawala wa jeshi la Ukraine, Oleg Synegubov, aliripoti kwenye Telegram kwamba moja ya makampuni katika jiji hilo ilipigwa na “makombora manne ya S-300” na moto ukazuka.

WATAKAO TUPA TAKA HOVYO NJOMBE MJINI KUCHUKULIWA HATUA KALI


Katika kuadhimisha siku ya Usafishaji Duniani Septemba 16,2023, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Njombe Ndugu Kuruthum Sadick amesema Halmashauri haitamvumilia mwananchi yeyote, atakayeonekana kuchafua mazingira kwa kutupa taka hovyo mitaani na kwenye maeneo yasiyo rasmi.


Akielezea umuhimu wa usafi na kutunza mazingira Mkurugenzi Kuruthum amesema kuwa, usafi ni afya na ukitunza mazingira yanakutunza hivyo kila mwananchi anawajibu wakuhakikisha anafanya usafi kwenye maeneo yanayomzunguka kutunza maeneo ya mabonde na vyanzo vya maji kwa kuacha kutupa takataka hovyo.


Akiwa eneo la bonde linalopita mtaa wa National Housing kata ya Njombe Mjini ,ametoa onyo kwa wananchi ambao wanatupa taka kwenye bonde hilo ambalo siyo dampo rasmi kwa ajili ya takataka nakusema Halmashauri imetenga eneo rasmi kwa ajili ya kutupa taka hivyo bonde hilo lisitumike kutupia taka.


“Tumeweza kujumuika kufanya usafi kwenye hili bonde ni wasihi wananchi kuacha kutupa taka kwenye bonde hili na yeyote atakayebainika hatua kali zitachukuliwa,na tufahamu kuwa kuna vyanzo vyanzo vya maji kwenye bonde hili na tunaelekea msimu wa mvua siyo afya kwa vyanzo vyetu vya maji maana maji haya yanatumika, Halmashauri ina magari yakukusanya taka kupeleka dampo tuache kabisa kutupa taka kwenye eneo hili ambalo siyo rasmi ”


Katika hatua nyingine amesema ili kuhakisha Mji wa Njombe unaendelea kubaki katika hali ya usafi ,Halmashauri ya Mji Njombe itaendelea kuhamasisha na kushiriki usafi wa pamoja kila mwezi ili kuwa kumbusha wananchi kuwa wanawajibu wakutunza mazingira na kufanya usafi mpaka kwenye maeneo yanayowazunguka majumbani.


“Usafi usiishie hapa tu,tufanye usafi hadi majumbani, hii itatukinga na magonjwa, kama kipindupindu”


Kwa upande wake Afisa Afya wa Mkoa wa Njombe Bi.Saada Milanzi amesema ili kuendelea kutunza mazingira Halmashauri zote za mkoa wa Njombe ziendelee kutumia sheria ndogo zilizopitishwa ili kuwawajibisha na kudhibiti utupaji taka kwenye maeneo yasiyo rasmi.


Aidha ametoa wito kwa wananchi kuitikia wito wakushishiriki shughuli za usafi na kutii sheria mbalimbali za usafi na utunzaji wa mazingira zilizowekwa na Halmashauri ili kuweka mazingira safi na kuzuia magonjwa ya mlipuko .


Naye mtendaji wa kata ya Njombe Mjini Enos Lupimo ameeleza mikakati waliyonayo katika kuweka eneo la Mji safi pamoja na kupambana na utupaji wa taka hovyo kwenye maeneo yasiyo rasmi kama kwenye mabonde.


“Sisi kama kata tunaenda kuunda kikosi kazi ambacho kitafanya kazi kuanzia ngazi ya mtaa ,kitahusu mazingira na afya,tutaoa elimu ya usafi na utunzaji wa mazingira na kisha tutaanza kuchukulia hatua wananchi ambao watakiuka sheria nakutupa taka hovyo kwenye mabonde na mitaani,tutakuwa na walinzi kwenye haya mabonde watafanya kazi usiku na mchana ,na ukionekana unatupa taka hovyo faini itahusika kwa mujibu wa sheria”.


Wadau mbalimbali ambao wameshiriki kuadhimisha siku hii ikiwemo taasisi ya SHIPO , Benki ya Taifa ya Uchumi (NBC),wanafunzi pamoja na vikundi vya vijana vinavyojishughulisha na mazingira ,wamesema jamii inatakiwa kutambua kuwa taka ni mali hivyo wanaweza kuzikusanya kwa utaratibu wakuzitenga taka ngumu zisizooza kama vile chupa za plastiki na zikatumika kwenye utengenezaji wa bidhaa mbalimbali.


Halmashauri ya Mji Njombe kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa mazingira pamoja na wananchi imeungana na nchi mbalimbali Duniani kuadhimisha siku ya usafishaji duniani kwa kufanya usafi kwenye maeneo mbalimbali ya Mji wa Njombe .

Sunday, May 27, 2018

KINGS FM TOP 30 MAY 27 KWA NGWARU BADO NI SHEEEDAH


Midundo mikali inasikika kila kona kwenye media tofauti tofauti duniani kote, Nchini Tanzania Media nyingi zimekuwa zikitumia siku za weekendy (Jumamosi na Jumapili) katika kuwasilisha Ngoma mbalimbali ambazo zinafanya poa katika chart kama Top 10, Top 20 na Top 30.

KINGS FM TOP 30 (01-15)

Kupitia Kings Fm Radio 104.3MHz Njombe Tz Radio ambayo pia waweza isikiliza kupitia king'amuzi cha Azam Tv Channel no 055 au kwa kupakua app ya Kings FM Radio kupitia simu yako ya Android (www.kingsfm.co.tz) hizi ndizo ngoma 30 kali kwenye Chart ya KINGS FM TOP 30.
KINGS FM TOP 30 (16-30)


Mpango mzima unaletwa kwenye redio yako Chini ya Lizrome Pouline chart imepangwa chini ya usimamizi wa Idara ya Muziki ikiongozwa na Teja wa Muziki Josee M'bongo, Sikiliza kuanzia saa 1200 - 1500 mchana.

Thursday, April 5, 2018

ZILIZOBAMBA



1. Kiongozi wa kambi rasmi ya upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, amezungumzia sababu za kukosekana kwa hotuba yake Bungeni na kusema Wamegomea Kusoma Hotuba Za Kambi Hiyo Kwa Wizara Yoyote Mpaka Watumishi Wa Ofisi Hiyo Watakaporejeshwa Kazini.
Freeman Mbowe

2. Moja kati ya stori inayoshika headlines kutoka nchini Libya ni hii kutoka Mahakama ya Tripoli ambayo imefuta kesi ya mauaji iliyokua ikimkabili Saadi Gaddafi, mtoto wa tatu wa aliekua rais wa Libya, Muammar Gaddafi.

Saadi Kaddafi amefutiwa mashtaka yote dhidi yake katika kesi ya mwanamichezo Bachir al-Rayani ambaye alifariki dunia mwaka 2006 baada ya kupigwa kichwani, Bachir Rayani alifariki dunia baada ya malumbano katika nyumba inayomilikiwa na Saadi Gaddafi.

3. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inatarajia kutoa uamuzi April 23,2018 kuhusu kesi ya kutumia dawa za kulevya inayomkabili mrembo Wema Sepetu na wenzake kama wana kesi ya kujibu au hapana na uamuzi huo unatarajiwa kutolewa na Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi watano wa upande wa mashtaka.

Mbali na Wema washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ya kutumia dawa za kulevya ni Angelina Msigwa  na Matrida Seleman Abbas.
Wema Sepetu


4. wasanii wengi kutoka Zanzibar wamekuwa waisahau fadhila na kusahau walikotoka hasa pale wanapohamishia majukumu yao kikazi Jijini Dar es Salaam, huyu hapa ni nedy music kutoka Zanzibar hapa anawajibu mashabiki wake ambao wanasema amekusahau kabisa Zanzibar.
Nedy Music

5. Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara amewataka Watanzania wawe wepesi wa kutoa pongezi pale wasanii wa filamu nchini Tanzania wanapofanya vizuri, na sio kuwabeza na kuwaponda kila siku kwani kitendo hicho kinawakatisha tamaa waigizaji wetu.
Haji Manara

Via ➡KingsFmRadio 104.3Mhz
      ➡KingsFmRadioAndroidApp 
      ➡Tunnein 12:00-12:15 pm
         www.kingsfm.co.tz

Monday, June 5, 2017

Breaking News: Halim Mdee na Ester Bulaya wapewa adhabu ya kutohudhuria Bungeni mpaka mwakani






Halima Mdee na Esther Bulaya wamehukumiwa kutohudhuria vikao vyote vya bunge linaloendelea mpaka mkutano ujao wa Bunge la Bajeti ya 2018/19.

Hukumu hiyo imeungwa mkono na wabunge wengi waliopitisha azimio hilo.

Mapema leo, Jumatatu Kamati ya Maadili  ilisema Bulaya na Mdee wamemaliza adhabu za kawaida zilizopo kwenye kanuni za bunge.

Hata hivyo, Bunge liliendelea  kujadili makosa ya wabunge hao wa Bunda na Kawe.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, George Mkuchika aliliomba Bunge kujadili adhabu inayostahili kulingana na makosa yao.

Kanuni inasema, mbunge anayefanya kosa la kwanza anaweza akazuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 10 na atayakosea kwa mara ya pili anaweza kuzuiwa kuhudhuria vikao visivyozidi 20.


Friday, April 14, 2017

Obby Claud Blog Tunakutakia Heri ya PASAKA


Bwana Yesu Asifiwe!
Tunamshukuru Mungu Baba kwa kutupa neema hii ya kushirikishana Neno la Mungu kwa Njia hii tena. Kesho tutakuwa tukiadhimisha sikukuu ya Pasaka, na makanisa mengi hivi sasa yapo kwenye majira ya kiibada ya Pasaka. Na Mungu ashukuriwe kwa kutupa neema ya kuadhimisha Pasaka katika mwaka huu wa 2012.
Wewe kama mwana wa Mungu, hupaswi tuu kuadhimisha Pasaka kwa mazoea, bali inakupasa na ni vyema sana kuadhimisha Pasaka kuanzia moyoni mwako, kwani Mungu anawatafuta watu watakaomwabudu katika roho na kweli.( Yohana 4:23 ), hivyo basi, napenda kwa msaada wa Roho Mtakatifu, tuyatafakari mambo machache kuhusu siku kuu hii ya Pasaka.
HISTORIA YA PASAKA
Katika Biblia, Pasaka ilianza kwa mara ya kwanza katika kitabu cha Kutoka 12, tafadhali tenga muda ukisome kitabu hiki kizima. Katika Pasaka hii ya kwanza, wana wa Israel waliagizwa kupakaa damu ya kondoo kwenye vizingiti vya juu na miimo ya milango yao kabla ya Mungu kuleta pigo la kumi kwa watu wa Misri, ambalo lilikuwa ni pigo la kuwauwa wazaliwa wote wa kwanza wa Wamisri.
Mungu aliagiza WaIsrael wapakae damu hiyo kwenye milango yao ili Malaika atakapokuwa anapita kuwaua wamisri, asiwaue na WaIsraeli pia. Na Malaika alipokuwa akipita, aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Wamisri, na aliacha kudhuru kila nyumba ya WaIsraeli, mradi tuu iwe imepakwa damu ya kondoo mlangoni.


DAWA ILIKUWA YA LAZIMA
Katika Kutoka 12:23, inasema “ BWANA apitapo katika nchi yote kuwapiga Wamisri, ataiona damu kwenye vizingiti na kwenye miimo ya milango naye atapita juu, wala hatamruhusu mwangamizi kuingia katika nyumba zetu na kuwapiga ninyi “. Jambo lililotakiwa hapa ili na Waisraeli wasipigwe, na wao kuweka damu kwenye milango yao. Bwana alichokuwa anaangalia si kuona kama nyumba fulani ni ya Muisrael au la, Yeye alikuwa anaangalia kama kuna damu mlangoni au la. Hii ina maana kuwa kama Mwisrael yeyote asingepakaa damu ya kondoo huyo katika mlango wake, angeangamia pamoja na Wamisri. Umeona msisitizo wa damu katika Pasaka hii ya kwanza? Na siku hiyo ndiyo siku ambayo wazaliwa wa kwanza wa Wamisri walikufa, na Waisraeli wote wakatoka utumwani Misri na kuanza safari ya kuelekea katika nchi ya Kaanani waliyoandaliwa na Bwana.
Na baada ya hayo, Mungu aliwaagiza WaIsrael kuiadhimisha siku hii daima na hata akasema “Watoto wenu watakapowauliza, ‘Sikukuu hii ina maana gani kwenu?’,Basi waambieni, ‘Hii ni dhabihu ya Pasaka kwa BWANA, ambaye alipita juu ya nyumba zetu alipowapiga Wamisri“( Kutoka 12:26-27 ). Kwa hiyo kuadhimisha Pasaka ni agizo la Mungu. Na pia Mungu akaendelea kusema “ Kwa sababu BWANA aliutenga usiku ule ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri katika usiku huu Waisrael wote wanapaswa kuadhimisha kwa kukesha ili kumheshimu BWANA katika vizazi vijavyo. ” (Kutoka 12:42 ).
Hivyo ndivyo namna Pasaka ilivyoanza kwa agizo la Mungu mwenyewe, na ukisoma katika Kutoka 12, ndivyo ilivyoendelea kuadhimishwa mara nyingi katika kipindi cha Agano la Kale. Kuna wakati wana wa Israel walikaa muda mrefu sana bila kuadhimisha Pasaka, lakini kila mara alipoinuka mtu aliyeisoma sheria ya Mungu, walitubu na kuendelea tena kuadhimisha siku hii ya Pasaka.
Kwa siku ya leo nimeona nikukumbushe namna Pasaka ilivyoanza ili usiwe unaadhimisha Pasaka kwa namna ya mwili tu, bali uadhimishe Pasaka kuanzia moyoni. Na ikitokea umeulizwa na mtu asiyeamini au asiyefahamu, basi uwe tayari kumweleza kwa upole kuhusu Pasaka. Nitakuletea sehemu ya pili ya somo hili ili kujifunza zaidi pia.


Thursday, March 23, 2017

Maneno ya Nape baada ya taarifa ya kutumbuliwa Uwaziri asubuhi hii




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo kwenye baraza la Mawaziri ambapo sehemu ya mabadiliko hayo ni kumteua Waziri mpya wa Habari, Sanaa, Utamaduni na michezo… na taarifa kamili ndio hii hapa chini kutoka IKULU.


Aliyekuwa Waziri wa Habari Nape Nnauye ameandika kupitia account yake ya Twitter ‘Ndugu zangu naomba TUTULIE! LEO mchana nitakutana na Wanahabari na tutalizungumza hili. Nitawaambia saa na mahali, kwasasa naomba TUTULIE!’



BREAKING: Rais Magufuli atengua Uwaziri wa Nape Nnauye





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo kwenye baraza la Mawaziri ambapo sehemu ya mabadiliko hayo ni kumteua Waziri mpya wa Habari, Sanaa, Utamaduni na michezo… na taarifa kamili ndio hii hapa chini kutoka IKULU.



Tuesday, March 21, 2017

Askofu Gwajima kutinga Clouds Media

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Gwajima aliandika....

"Taarifa: Kesho 22/03/2017 saa nne kamili asubuh nitakwenda Clouds Media kuwapa pole kwa yaliyotokea"



Tundu Lissu amtumia waraka Rais Magufuli

Tundu lisu amemwandikia waraka huo mhe. Rais wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Jonh pombe magufuri akiwa kama raisi wa Tanganyika Law Society (TLS).

Usome waraka hapa chini



Monday, March 20, 2017

Tanzania, Rwanda na Burundi Kati ya Nchi Zenye watu wasio na Furaha duniani.

Tanzania Rwanda na Burundi zimeorodheshwa kuwa kati ya nchi zenye watu wasio na furaha duniani.
Rwanda iko nafasi ya 151 , Tanzania nafasi ya 153 huku Burundi ikiwa nafasi ya 154 kati ya nchi 155.

Norway ndiyo imechukua nafasi ya kwanza kama nchi yenye watu walio na furaha zaidi duniani, kwa mujibu wa ripoti ya Umoja wa Mataifa na kumshinda jirani wake Denmark, ambayo ichukua nafasi ya kwanza mwaka uliopita.

Ripoti hiyo inaangazia furaha watu waliyo nayona ni kwa nini.
Uhaba mkubwa wa wafungwa waikumba Uholanzi
Kuwa na mpenzi na afya nzuri huchangia furaha
Bia husaidia watu 'kufungua roho'
Watanzania hutafuta nini mtandaoni?
Denmark, Iceland, Uswisi na Finland zinachukua nafasi tatu za kwanza huku nchi ya Jamhuri ya Afrika ya katika ikichukua nafasi ya mwisho kati nchi zenye watu wasio na faraha duniani.

Mataifa ya magharibi mwa Ulaya na Marekani pia nayo yako na watu wenye furaha duniani wakati Marekani ikichukua nafasi ya 14 na Uingereza nafasi ya 19.

Wezi 13 wajinga zaidi duniani
Nchi zilizo kusini mwa jangwa la Sahara na zile zinazokumbwa na mizozo, zina alama za chini. Syria ilichukua nafasi ya 152 kati ya nchi 155 huku Yemen na Sudan Kusini, nchi zinazokumbwa na njaa zikichukua nafasi za 146 na 147.

Source: BBC



Magufuli asema Makonda chapa kazi



Tofauti na kile ambacho watanzania wengi leo walikuwa wakitarajia kuona Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Dkt John Magufuli akichukua uamuzi mgumu dhidi ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, mkuu huyo wa nchi amemuelezea Makonda kuchapa kazi.

Makonda anakabiliwa na kashfa lukuki ikiwemo ile ya kudaiwa kughushi vyeti na kwamba jina lake halisi ni Daudi Bashite, kutumia vibaya madaraka yake ikiwemo tukio la juzi la kuvamia studio za Clouds Media Group akiwa na wanajeshi wenye silaha akilamizimisha kurushwa kwa kipindi na zingine. Tukio hilo limelaaniwa vikali.

Akizungumza Jumatatu hii kwenye uwekaji jiwe la msingi katika mradi wa barabara za juu (Flyovers) Ubungo, Dar, Rais Magufuli amesema, “Mimi ndio najua mwenyewe nani anatakiwa kuwa wapi akae wapi, ni mimi ninayepanga. Ninajua wamenielewa. Kwahiyo Makonda wewe chapakazi, nasema chapa kazi.”

“Suala la kuandikwa kwenye mitandao sio tija kwangu, hata mimi ninaandikwa kwenye mitandao kwahiyo nijiuzulu urais? Chapa kazi, hapa kazi tu.”

Rais amesema Watanzania wanapoteza muda mwingi kwa mambo yasiyo ya msingi.

“Tumepoteza direction tumeanza kujadili personalities,” aliongeza.


Nape asema Kitendo Kilichofanywa na Mkuu wa Mkoa kimenajisi Tasnia ya Habari




Waziri Nape: Kabla ya kuchukua hatua zozote, sisi kama Serikali tunataka kusikia kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda

Waziri Nape: Tumeunda timu ya watu 5 kufanya kazi katika saa 24 ili wapate maelezo ya RC Makonda na ripoti hiyo itasomwa wazi

Waziri Nape: Kitendo kilichofanywa na RC Makonda kinanajisi Uhuru wa Vyombo vya Habari katika Nchi Huru. Mamlaka zitajua cha kufanya

Kusaga: Kama RC Makonda ataomba radhi hatuna shida naye, ataendelea kuwa rafiki!

Reginald Mengi: Tuna Rais anayependa Vyombo vya Habari, lakini mapenzi haya ayaonyeshe kwa Vitendo!

Nape Nnauye(Waziri wa Habari): Wanahabari tutulie na tusubiri kusikia kutoka pande zote mbili kabla ya kuchukua uamuzi

Nape: Natoa pole kwa Clouds Media na kwakuwa tumejiridhisha kuwa jambo hili limetokea basi tutalishughulikia

Nape Nnauye: Ripoti itakayoletwa na Kamati ya Uchunguzi pamoja na hatua zitakazochukuliwa vitatangazwa hadharani baada ya saa 24\

Habari zaidi....

Waziri Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye amesema kuwa Tukio la Uvamizi wa Kituo cha Habari cha Clouds unaodaiwa kufanywa na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Paul makonda akiwa na askari kadhaa ni tukio la kupingwa huku akidai kuwa matukio kama hayo hutokea pindi nchi inapotaka kupinduliwa lakini kama Rais yupo, nchi haijapinduliwa.

Aidha amesema kuwa Vitendo hivyo ni kunajisi uhuru wa habari na kama akishindwa kusimamia hilo na yeye hafai kuwa katika nafasi aliyopo.

Chanzo : Mwananchi


New Posts

IJUE SCANIA P380[Mende]

Scania P380 Mende ni nini? Scania P380 ni mojawapo ya malori maarufu yaliyoundwa kwa nguvu na ufanisi wa hali ya juu, hasa kwa mazingira ya ...